Ads

AMANI NITUNU KWA TAIFA LETU TUSIKUBALI MACHAFUKO



Na mwandishi wetu

Dar es Salaam 

MGOMBEA mweza wa Urais kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi,Evaline Wilbard Munisi amewataka watanzania kudumisha amani iliyopo nchini kwamba Amani ya Taifa letu ni dhamana yetu sisi wenyewe,amani ikipotea hakuna pakuipata.


Akizungumza  Leo Oktoba 4,2025katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni   Jimbo la Kibamba  zilizofanyika katika eneo la Stendi ya Magufuli Jijini Dar es Salaam amesema kuwa  tulinde amani yetu tumeiasisi kutoka enzi na enzi tusishawishike Wala kudanganyika na wanaoleta uchochezi na ushawishi Kwa ajili ya machafuko na ghasia.


"Amani ya Taifa letu ni dhamana yetu sisi wenyewe,amani ikipotea hakuna pakuipata,nchi tulizopakana naizo zote wanakimbilia kwetu,Sasa sisi kikinuka  kama ambavyo wanasema watakinukisha hatuna pa kwenda,tuilinde amani yetu tumeiasisi kutoka enzi na enzi msishawishike Wala msidanganyike na wanaoleta uchochezi na ushawishi kwa ajili ya machafuko na ghasia",amesema


Amani ya nchi ndio dhamana ya mwananchi mwenyewe lakini wewe mwenyewe usishawishike tumejipanga kuanzisha mijadala ya amani,mijadala ya muafaka na itaanzia ngazi ya kata,Jimbo Hadi Taifa na vijana watashiriki kikamilifu na kutakua na utaratibu na masharti  mepesi kwa vijana kujiunga na jeshi la kujenga Taifa(JKT) kwani ili kuwajenga vijana kuwa wakakamavu na maadili mema sasa hivi tunaona mmomonyoko wa maadili  na wakulaumiwa ni sisi wazazi kwa sababu vijana tumewaacha  na kuwasahau na masharti yamekuwa mengi pamoja na vigezo vingi ambavyo vinawashinda kujiunga huko,endapo NCCR-Mageuzi kitashika dola watahakikisha vijana wote wenye sifa watajiunga bila kujali umri kikubwa ni vijana wawe na maadili kwani mafundisho wanayoyapata yanawajenga kuwa wazalendo na  watii.


Aidha ,amesema kwamba wananchi wakichague chama Cha NCCR- Mageuzi kwa kumpigia kura  Mgombea Urais Ambar Haji Khamis ,huku akimnadi Mgombea Ubunge Jimbo la Kibamba ,Lightness Laizer pamoja na mgombea Udiwani wa Kata ya Mbezi,Talick Abdul Rahman Saad.


Kampeni hizi ni muendelezo wa kampeni  zinazoendelea kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29,2025 huku akiwataka wananchi kukipa ushindi wa kishindo chama hicho wagombea wao kwa nafasi ya urais,ubunge na Udiwani


Mgombea Mwenza Munisi amesema kwamba tunataka kuona mageuzi katika suala Zima la Uchumi Jumuishi ambapo tutajumuisha wananchi wote wenye sifa  watashiriki harakati za kiuchumi katika maeneo yote  ili kuingiza Pato la Taifa pamoja na wananchi wanufaike  katika ajira za muda mrefu na mfupi na watakaopata  ajira za kudumu kulingana na weledi na elimu na sifa  zinazohitajika mahali hapo.

"Hatutaruhusu wageni waje kunufaika na maeneo yetu ya vitega uchumi kwani  wazawa wanapaswa kunufaika lakini mnawekewa masharti magumu hata Kodi mnashindwa wanakuja kunufaika wageni badala ya wazawa.


Sanjari na hayo amesema kwamba tutahakikisha watanzania wananufaika na maliasili zilizopo kwani tutaboresha na kuvumbua maliasili  ili ziwanufaishe watanzania na si mafisadi.


Sambamba na hayo pia amesema kwamba wataboresha huduma ya afya ya mama na mtoto pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa dawa katika hospitali na kuboresha maslihi ya wauguzi  na madaktari ili kukomesha mazingira ya kuomba rushwa huku mishahara ikitoka kwa wakati na kuongezeka Kila mwaka.


Aliendelea kwamba watahakikisha wanaboresha maslahi kwa vyombo vya ulinzi na usalama kwa kuwawekea mazingira mazuri ya kuishi kwa hadhi yake na cheo chake.


Alimalizia kwa kusema kwamba  endapo NCCR- Mageuzi watapata ridhaa ya kuongoza nchi hii watahakikisha Jimbo la Kibamba kupitia Mbunge wao watajenga soko kubwa ili kuwarahisishia wakazi wa eneo Hilo na  wafanyabiashara kufanya biashara zao kwa urahisi pamoja  kuhakikisha Barabara zinakuwa na lami.


Kwa upande wake Mgombea Ubunge Jimbo la Kibamba ,Lightness Laizer amesema kwamba atahakikisha anatekeleza Ilani ya Chama hicho pamoja na kuboresha  maisha ya wananchi .


Aidha amesema kwamba kumekuwa na changamoto kubwa ya afya ya akili hii inasababishwa na ugumu wa maisha Kwa watu kubaka,ukatili na kujiua kitu ambacho akili inafikia muda haifanyi kazi vizuri hivyo mkinipa ridhaa chama hiki tutaboresha  maisha na kukomesha ukatili


Naye Mgombea Udiwani  Kata ya Mbezi,Talick Abdul Rahman Saad amesema kwamba endapo mtanipa ridhaa yakuwa diwani nitahakikisha changamoto za Barabara,maji na afya zinatekelezwa lakini pia nitahakikisha na kusimamia fursa za vijana na kukuza vipaji vyao







No comments