Ads

TIC YA MKABIDHI HATI YA KUJENGA KIWANDA MWEKEZAJI ALIYEPATA ENEO KWA PROPERTY INTERNATIONAL.



Na John Luhende 

Mwamba wa habari 

Kituo Cha uwekezaji nchini  TIC kimesema  kimeweka mazingira Bora ya uwekezaji nchini jambo ambalo limesaidia kuvutia wawekezaji kuwekeza kwaa wingi.

Hayo yamebainishwa na Afisa uwekezaji na msimamizi wa dawati la Mashariki ya kati Bwana Juma  Nzima  akizungumza  wakati alipokuwa anakabidhi  hatimiliki   kwa Mwekezaji  wa kampuni ya Vax Industries Ltd (Packaging Industries katika Banda la TIC katika maonesho ya biashara ya 48 ya yanayoendelea Jijini Dar es salaam.

Aidha ameitaka sekta binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali kupitia kitu hicho kuweka akiba ya Benk ya ardhi  katika maeneo yaliyo rasimishwa  kwaajili ya uwekezaji .

"Leo tumefanikisha kutoa hati isiyo asili kwa Mwekezaji anayewekeza maeneo ya Kigamboni Kisarawe Il ,  kiwanda Cha kuchakata vifungashio na eneo hili limetoka sekta binafsi katika kampuni ya Property International tunawashukuru Sana kwaushirikiano wao kwa kuleta maeneo yao na tukayatangaza  kwa wawekezaji" Alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni ya uuzaji viwanja ya Property International ambao ndiyo wametoa  eneo la kiwanda kwa Mwekezaji huyo  Bwana Abdlharim Zahran , ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuweka mazingira Bora na wezeshi kwa wawekezaji.

"Wawekezaji hawa hawaji kwa bahatimbaya mazingira yalipo ndiyo yanayowavutia kuja kuwekeza ndani ya nchi yetu na TIC wamejipanga vizuri hata Leo sikutajia  kama hati hii  itaweza kukabidhidhiwa ndani ya  maonesho katika viwanja vya  Sabasaba "Alisema.

Vilevile ametoa wito kwa sekta binafsi wenye miradi Yao  kupeleka na kuisajili  TIC kunamsaada mkubwa Sana  kwa sababu wewekejaji wengi wamehamasishwa  kuwekeza Tanzania na wanafika TIC  kupata taarifa za uwekejaji .

"Unapo sajili miradi yako TIC Wana kutafutia mteja kazi inaenda kwa haraka Sana  na Imani na Serikali  imekuwa kubwa Sana"Alisema Mkurugenzi huyo.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya Vax Industries Ltd iliyo pewa hati miliki ya eneo kiwanda kutoka Property International Bwana  Viswa  Vardhan Reddy ,  amekishuku kituo Cha uwekezaji TIC kwa kufanikisha kuwaunganisha na Property International na kupata eneo la kujenga kiwanda  ambapo  ameahidi kuwa karibu wataanza ujenzi . 

No comments