IBADA YA KUSIFU, KUABUDU NA MAOMBEZI YALETA AHUENI KATIKA KANISA LA MORAVIANI JIMBO LA MASHARIKI, USHIRIKA WA MBEZI LUISI
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa
la Moraviani Jimbo la Mashariki, Ushirika wa Mbezi Luisi, Mchungaji Timothy
Mwankenja akiwaombea wajumbe wa Kamati ya maandalizi ya ibada Maalamu ya
Kusifu, Kuabudu na Maombezi. Ibada hiyo inafanyika kila mwezi katika
kanisa hilo.
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa
la Moraviani Jimbo la Mashariki, Ushirika wa Mbezi Luisi, Mchungaji Timothy
Mwankenja akiwaombea waumini wa kanisa hilo katika ibada Maalamu ya Kusifu, Kuabudu na
Maombezi baada ya kukubali kuoka na kuacha maisha ya kutenda dhambi katika
maisha yao.
Baadhi ya waimba wa Kanisa la
Moraviani Jimbo la Mashariki, Ushirika wa Mbezi Luisi wakitoa huduma katika ibada
Maalamu ya Kusifu, Kuabudu na Maombezi iliyofanyika siku ya jumapili ya tarehe
17/7/2022 katika hilo lililpo Mbezi jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya waumini wa Kanisa
la Moraviani Jimbo la Mashariki, Ushirika wa Mbezi Luisi wakiwa katika maombi ya ibada Maalamu ya Kusifu, Kuabudu na Maombezi iliyofanyika siku ya
jumapili ya tarehe 17/7/2022 katika hilo lililpo Mbezi jijini Dar es Salaam.
(Picha na Noel Rukanuga)
NA NOEL RUKANUGA, DAR ES
SALAAM.
Watanzania wametakiwa
kuondokana na utamaduni wa kusali kwa mazoea badala yake wanapaswa kumuabudu
Mungu katika roho na kweli jambo ambalo litawasaidia kuepukana na changamoto
pamoja na kupiga hatua katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo.
Akizungumza katika ibada
Maalamu ya Kusifu, Kuabudu na Maombezi iliyofanyika siku ya jumapili ya tarehe
17/7/2022 katika Kanisa la Moraviani Jimbo la Mashariki, Ushirika wa Mbezi
Luisi, Mchungaji Kiongozi wa kanisa hilo, Mchungaji Timothy Mwankenja, amesema
kuwa ibada ya kweli ni ulinzi kwa kila mtu anayemwamini Mungu.
Mchungaji Mwankenja,
amesema kuwa kumuabudu Mungu ni kuwa na ushirika na yeye katika kuhakikisha
unakuna na mawasiliano mazuri kupitia sala na maombi.
Amesema kuwa ukisoma
kitabu cha nabii Yohane 3 : 16 kimeeleza Mungu aliacha Mbingu na nchi kwa sababu
ya kuwapenda wanadamu, hivyo tumeubwa ili tuwe na ushirika na Mungu.
“Tumeubwa kwa mfano wa sura
ya Mungu, tuache kujinenea mabaya, binadamu aliyeubwa kwa mfano wa Mungu anafanikiwa
katika jambo lolote, tumuabudu kwa uzuri na utakatifu” amesema Mchungaji Mwankenja.
Amesema kuwa Roho Mtakatifu
ni mwaminifu katika maisha yetu ya kila siku, lakini vipo baadhi ya vitu
ambavyo tumejiwekea sisi wanadamu katika utaratibu wa kumuabudu Mungu, lakini
sio vya kweli mbele yake.
Amesema kuwa tunapaswa
kuishi kwa kutumia vipawa vyote ambavyo Mungu amekupa katika maisha yako ili
ukifa uwe umetimiza kusudi la Bwana na kutofanya hivyo ni vibaya kwani
umeshindwa kutimiza kusudi la lake.
“Mungu ndani yako aliweka
maono uwe aidha uwe tajili, ulikomboe Taifa, umiliki viwanda, lakini ukifa bila
kuonesha kipawa chako tutalia kuliko msiba wenyewe, na kuwepo duniani bila
kumuabudu Bwana aliyekuumba ili umuabudu hiyo ni mbaya kuliko kitu kingine
chochote ” amesema Mchungaji Mwankenja.
Mchangaji Mwankenja ameeleza
kuwa anatamani kuona kila mtu anamwabudu katika roho ya kweli na kuondoka
katika ibada ya maigizo na kuacha kabisa kumuabudu Mungu katika mwili.
Amesema kuwa hakuna kitu
ambacho kinaweza kuzuia mkono wa Mungu, hivyo tuna kila sababu ya kujiepusha na
mambo yanahusu Mungu katika kuongea kinyume.
Mwenyekiti wa Kamati ya
Maandalizi ya Ibada ya Kusifu, Kuabudu na Maombezi, Kanisa la Moraviani
Ushirika wa Mbezi Luisi, Dkt. Oswald Masebo, amesema kuwa kupitia ibada ya kusifu
na kuabudu ambayo inafanyika mara moja kila mwezi wameendelea kuinuliwa kiimani
na kuwa karibu na Mungu.
Dkt. Masebo amesema kuwa
ibada hiyo imekusudiwa ili wakristu wapate neema ya kumuabudu Mungu kwa
kumsifu, kufanya maombi pamoja na watu wenye shida mbalimbali wapate nafasi ya
kuombewa.
“Kuna huduma ya maombezi kwa
watu wenye shida mbalimbali kusudi Mungu aweze kushughulika na mahitaji yao
ndani ya ibada ya kusifu, kuabudu na maombi” amesema Dkt. Masebo.
Ameeleza kuwa katika ibada
hiyo wakristu wamepata nafasi ya kuliombea Taifa, kanisa, familia zao pamoja na
kumshukuru Mungu kwa neema ambayo ameendelea kuwapa kanisa hilo pamoja
na watu wake.
Dkt. Masebo amefafanua
kuwa lengo kubwa la ibada ya kusifu, kuabudu na maombi ni kumtukuza Mungu ili
yeye mwenyewe ajitwalie utukufu wake.
“Nimepata neema ya kumtumikia
Mungu kama Mwenyekiti wa Kamati ya kuandaa ibada maalumu ya kusifu, kuabudu na
maombi, lakini maono anayo Mungu Mwenyewe kwa sababu huduma tunayofanya sio ya kwetu binafsi ni ya
Mungu Mwenyewe” amesema Dkt. Masebo.
Amesema kuwa Mungu Mwenyewe
anaendelea kuachilia maono na mawazo ya kila mwezi namna ambavyo ibada inapaswa
kufanyika.
Ameeleza kuwa wanaendelea
kumuomba Mungu kwani ibada hiyo ni dalili za muamusho mkubwa ambao unaendelea kuchukua
nafasi katika makanisa mbalimbali.
Hata hivyo waumini wa
kanisa la Moraviani Jimbo la Mashariki, Ushirika wa Mbezi Luisi wamemshukuru
Mungu kwa maono ya kushiriki ibada ya kusifu, kuabudu na maombezi kutokana imeendelea
kuwa baraka katika maisha yao.
Bi. Kumbuka Luwondo, amesema
kuwa anamshuku Mungu kwa sababu katika ibada hiyo wameona mabadiliko ya
kujifunza namna ya kumtumika Mungu, ibada halisi na kusongea katika viwango vya kuomba kwa muda mrefu.
“Tumepata muda mzuri ya
kumuabudu Mungu, kusifu na kuabudu na watu pia wamepata nafasi ya kuokoka na
kutengeneza maisha yao mpya jambo ambalo katika ibada nyengine sio jambo la
kawaida” amesema Bi. Luwondo.
Ibada ya kusifu, kuabudu na
maombi Kanisa la Moraviani Jimbo la Mashariki, Ushirika wa Mbezi Luisi inafanyika
mara moja kila mwezi katika Kanisa la Moraviani Jimbo la Mashariki, Ushirika wa
Mbezi Luisi ambapo waumini wa kanisa hilo wanapata fursa kumuimbia Mungu pamoja
na kufanya maombi mbalimbali ikiwemo kuliombea Taifa.
Post a Comment