Ads

WADAU WAPIGWA MSASA KUHUSU BIASHARA YA FOREX

Forex no biashara ya ubadilishaji wa fedha za kigeni ambao imeonekana kuwa na mzunguko mkubwa zaidi kuliko biashara yoyote duniani kwani inazungusha zaidi ya dolla za kimarekani trilioni 5 kwa siku. 

Hii ni biashara ambayo imechangiwa sana na mapinduzi ya teknolojia ambayo sasa mtu yoyote anaweza kufanya biashara hiyo ambapo kuna mtandao wa internet kama kompyuta na simu janja (Smartphone).

Kwa kutambua hilo kampuni ya udalali wa biashara ya forex,(Vault Market Tanzania)ambayo hutengenezwa platform kwa wanaotaka kufanya(wanaofanya) biashara hiyo imemleta hapa nchini mfanyabiashara maarufu na mwenye mafanikio kupitia biashara hiyo Joash Naidoo kwa lengo la kutoa elimu juu ya biashara ya forex.

Akizungumza na waandishi wa habari katika semina maalum iliyolenga kukuza uelewa juu ya biashara ya forex hapa nchini Bw. Ezra Yoyo, amesema ili uweze kuingia kwenye biashara ya forex ni lazima utumie 'brockers' uweke pesa na uanze biashara (ku trade)na kampuni ya Vault Market ni moja ya brockers waliopo hapa nchini.

Amesema kampuni ya Vault Markets yenye makao yake makuu nchini Afrika ya kusini tayari imefungua matawi katika miji mbalimbali mikubwa katika nchi nchi tofauti barani Africa ikiwemo Namibian na sasa jijini Dar es salaam nchin Tanzania na wana mpango wa kuenea majiji yote hapa nchini.

Akizungumzia semina hiyo, amesema wameamua kumleta Joash Naidoo ambaye ni forex trader mwenye mafanikio makubwa ili kuja kuwaambia ukweli watanzania juu ya biashara hiyo na jinsi alivyopata mafanikio kupitia kampuni ya brockers ya Vault Market ambayo ilimpa platform ya kuifanya biashara hiyo ambapo mpaka sasa anafanya.

Aidha amesema kuwa semina hiyo imekuwa na mafanikio makubwa na amewataka watanzania kujiridhisha na biashara ya forex kwani ni moja ya biashara zenye mafanikio makubwa endapo wataitumia kampuni ya Vault Market kama brockers wa 'forex trade'.

No comments