Ads

MANISPAA YA KIGAMBONI YAPATA MEYA



Msimamizi wa uchaguzi wa Meya Manispaa ya Kigamboni  Dalmia  Mikaya Tumaini ambaye ni katibu tawala wa Wilaya ya Kigamboni amemtangaza  Ernest Mafimbo Ndamo Diwani wa Kata ya Tungu kuwa Meya wa Manispaa .



Mafimbo amechukua nafasi hiyo baadaya ya kupata kura  zote 13 kati ya kura zilizopigwa  na Madiwani wa kata tisa Mbunge na Madiwani watau wa viti maalumu, kwa upande wa  Naibu Meya amechaguliwa Stephano Maganga  Waryoba, naye kadhalika  amepata kura zote 13 .

Akizungumza baada ya kuchaguliwa katika nafasi ya Mstahiki Meya Ernest Mafimbo amewataka Madiwani kufanya kazi kwa ushirikiano na watumishi wa Manispaa ili kuweza kutimiza majukumu yao ya kazi.

"Nashukuru kwa kunipa imani kubwa nami nawaahidi kuwa nitawatumikia pia nita tenda haki kwa madiwani wote bila ubaguzi  wa aina yoyote ,tunaelekea hatua nyingine baraza lililopita lilikuwa  makini likijadili  mijadala kwa kuzingatia nguvu za hoja ,   niombe baraza hili  tuuendeleze utamaduni huo"amesema.

Naye naibu meya Stephano Maganga  Waryoba, akitoa salamu za shukrani amesema atakuwa mshauri mzuri kwa kwa viongozi na kuleta tija na atakuwa tayari kupokea maelekezo kutoka kwa viongozi wake.

Kabla ya uchaguzi huo Madiwani wateule wa Manispaa ya Kigamboni,  walikula kiapo cha uaminifu na maadili , rasmi kwa kuanza kutekeleza majukumu yao ya  uwakilishi wa wananchi Katika Manispaa na utekelezaji wa shuguli za Maendeleo.

Baada ya Meya na Naibu Meya kuongea na kutoa shukranizao Katibu Tawala alipata wasaa wa kuzungumza na madiwani hao ambapo amesema  wananchi wamewaamini na serikali imewaamini  amewataka kwenda kuwasikiliza na kutatua kero za wananchi kwa kuzingatia maslahi ya taifa na mkatenge siku zenu maalum hata maramoja kwa mwezi kukaa na kuzungumza na wananchi wenu .

"Waheshimiwa Madiwani mlio kula kiapo leo nawahidi kuwa tutashirikiana" Mikaya.


No comments