Ads

WIZARA YAWARUHUSU VIONGOZI WA MATAWI YANGA KUFANYA MKUTANO.



Hatimaye viongozi wa Matawi wa Klabu ya Yanga wamepata kibali kufanya mkutano wao katika makao makuu ya klabu hiyo.

Kibali maalum kimetolewa na Wizara ya Mambo ya Ndani kuwaruhusu YAnga kufanya mkutano wao siku watakayokuwa wamepanga.

Awali, Jeshi la Polisi lilizuia mkutano wa viongozi hao wa Matawi wa Yanga uliokuwa ufanyike klabu hapo siku tatu zilizopita.

Lakini sasa, wizara hiyo imeandika barua na kusisitiza mkutano huo kuwa na manufaa kwa ajili ya klabu hiyo pia soka la Tanzania na si vinginevyo.

No comments