TRA YASEMA MAKUSANYO YA KODI KWA KIPINDI CHA NUSU MWAKA ,YAMEPANDA HADI TRILION 7.87
Richard Kayombo mkurugenzi wa (TRA) Elimu kwa walipakodi
Mwambawahabari
MAMLAKA ya Mapato
Tanzania (TRA) imesema , imevunja rekodi ya makusanyo katika kipindi cha miezi sita ya
mwaka wa fedha 2017/2018 Julai hadi Desemba 2017 kwa kukusanya
sh.trilioni 7.87
Akizungumza na
waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Huduma na Elimu wa
kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo, amesema makusanyo hayo ni makubwa
ukilinganisha na kipindi kama hicho kilichopita.
“Katika kipindi cha
miezi sita ya mwaka wa fedha 2017/2018 yaani kuanzia Julai hadi Desemba 2017,
TRA imekusanya jumla ya sh.trilioni 7.87 ikilinganishwa na sh.trilioni 7.27
ambazo zilikusanywa kipindi kama hicho katika mwaka wa fedha 2016/2017 ambacho
ni sawa na ukuaji wa asilimia 8.45,” amesema Kayombo.
Ameongeza, katika
mwezi wa Desemba 2017 pekee, TRA imekusanya sh.trilioni 1.66 ikilinganishwa na
makusanyo ya Desemba 2016 ambapo ilikusanya sh.trilioni 1.41 ambayo ni sawa na
ukuaji wa asilimia 17.65.
Post a Comment