Serikali Yapongezwa kwa Kuwaleta Pamoja wadau wa Mazingira na Wazalishaji Mifuko ya Plastiki
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
 Rais,Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akifungua Kikao cha 
Wazi cha kupokea maoni ya wadau kuhusu dhamira ya Serikali kupiga 
marufuku uzalishaji,uuzaji,usambazaji na matumizi ya mifuko ya plastiki 
leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa 
Rais Prof. Faustine Kamuzora akiongea wakati wa ufunguzi wa Kikao hicho 
leo Jijini Dar es Salaam.Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa 
Rais,Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba.
Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard  Muyungi akiongea wakati wa Kikao hicho mapema leo.
Mwenyekiti wa Umoja wa 
wazalishaji wa mifuko isiyo na athari kwa mazingira Bw. Jumanne Mgude 
akionesha mfuko unaozalishwa hapa nchini usio na athari kwa mazingira 
wakati wa Kongamano hilo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya
 Wande Printing and Packaging (T) Ltd Bw. Joseph Wasonga akitoa maoni ya
 wamiliki wa Viwanda vya Kuzalisha mifuko ya plastiki hapa nchini wakati
 wa kikao hicho. 
Katibu wa Umoja wa wazalishaji wa
 mifuko isiyo na athari kwa mazingira Bw. Sadick Mgonge akitoa maoni ya 
umoja huo wakati wa Kikao hicho leo.
Sehemu ya wadau walioshiriki kikao hicho leo Jijini Dar es Salaam wakifuatilia mjadala na maoni ya washiriki .
 (Picha zote na Frank Mvungi-Maelezo)
…………………………………………………………………………………………….
Frank Mvungi-Maelezo
Wadau wa Mazingira  na 
Wazalishaji wa Mifuko ya Plastiki hapa nchini wameipongeza Serikali kwa 
kuwakutanisha pamoja ili kujadili kuhusu matumizi ya mifuko ya plastiki 
na kutoa maoni yao kwa Serikali juu ya kuchukua hatua kwa mujibu wa 
Sheria ya Mazingira.
Akizungumza wakati akifungua 
 kikao cha wazi cha kupokea maoni ya wadau kuhusu dhamira ya Serikali 
kupiga marufuku uzalishaji, uuzaji, usambazaji na matumizi ya mifuko ya 
plastiki, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira 
 Mhe. January Makamba amesema dhamira ya Serikali ni kupata maoni ya 
wadau na wazalishaji wa mifuko hiyo ili Serikali ifanye tathmini kabla 
ya kuchukua hatua na kuweka mazingira yatakayowezesha utekelezaji wa 
Sheria ya Mazingira kwa kila mdau.
“Changamoto imekuwa kubwa katika 
matumizi ya mifuko ya plastiki katika swala la mazingira kwani 
tumeshuhudia miundo mbinu yetu ikiathirika, mifugo na hata viumbe vya 
baharini na kwa mujibu wa tafiti kuna hatari baadae mifuko hii ikawa 
mingi zaidi baharini kuliko samaki” Alisisitiza Makamba.
Akifafanua Makamba amesema kuwa 
Serikali imeona ni vyema ikakutana na wadau ili ipate maoni yao kwa 
kuzingatia kifungu cha 178 cha Sheria ya Mazingira kinachotaka wananchi 
na wadau kushirikishwa na kupata taarifa kuhusu maswala ya mazingira.
Aliongeza kuwa kuanzia sasa Ofisi
 yake itakuwa ikishirikiana na wadau katika mambo yote yanayohusu 
mazingira ili kuongeza tija na kutoa fursa kwa wadau hao kutoa maoni 
yatakayosaidia katika usimamizi wa Sheria na Kanuni.
Naamini kutakuwa na kuvumiliana 
wakati wa kutoa maoni ili Serikali ipate maoni ya wadau wote kwa ufasaha
 na hii itasaidia Serikali katika kuchukua hatua ikiwemo kuhakikisha 
kuwa kuna usimamizi dhabiti wa Sheria ya Mazingira.
Pia Waziri Makamba alilitaka 
Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kusimamia Sheria ya 
Mazingira kikamilifu ili kulinda rasilimali za Taifa.
Kwa upande wake Naibu Mwenyekiti 
wa Chama cha Wazalishaji wa Plastiki Tanzania Bw. Ahmed Abdallah 
amepongeza utaratibu huo wa Serikali kukutana na wadau.
Kumekuwa na maoni mbalimbali 
kuhusu matumizi ya mifuko ya plastiki huku baadhi ya wadau wakidai 
imekuwa na athari kubwa katika mazingira zikiwemo magonjwa, uharibifu wa
 miundo mbinu na kuleta mabadiliko ya tabia nchi .
Post a Comment