Watanzania waondolewa hofu ya kusoma nchini India
Na: Frank Shija,
mwambawahabariblog
Watanzania wahasishwa
kujiunga na masom katika Vyuo na taasisi za masomo zilizopo nchini India kwaku
kuna fursa nyingi za kupata elimu na ni nchi salama kwa wageni waishio nchini
humo.
Rai hiyo imetolewa jana
jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa EdCIL (India)
Limited, Bw. Diptiman Das wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu
Kampeni ya kuhamasisha Watanzania kusoma nchini India ijulikanayo kama Study
in India Campaign iatakayofanyika katika ukumbi wa Mlimani City
kuanzia tarehe 18 hadi 19 Februari.
Diptiman amesema kuwa
kupitia Kampeni hiyo Watanzania watapata fursa ya kuunganishwa na Vyuo vikuu
zaidi ya 712 vyuo vya kati 36671 na Taasisi zaidi ya 11445 zinazotoa
taaluma katika fani za Uhandisi,Udaktari,Famasia, Nesi, Uongozi, IT,
Bio-technology, Media Studies, Kilimo na Hotel Management
Kwa upande wake Balozi
mdogo wa India hapa nchini Robert Shetkintong amesema kuwa India imekuwa
ikisaidia Serikali ya Tanzania katika mafunzo mafupi kwa watumishi wa umma
ambapo kila mwaka karibu wafanyakazi 300 wa Serikali upelekwa India kwa ajili
ya mafunzo mafupi.
Aidha Balozi huyo
amewatoa hofu Watanzania kuwa India ni mahali salama kwa kusoma pamoja na
changamoto zilizojitokeza za baadhiwanadunzi wa Kitanzania kupata usumbufu na
kuongeza kuwa hali hiyo inawezakujitokeza sehemu yeyote na siyo jadi ya nchini
mwao na kuwahakikishia Watanzania kuwa hali ya kiusalama ni shwari.
EdCIL ni Taasisi
inayojiendesha kwa faida imesajiliwa kwa na kupata cheti cha
Serikali ya IndiaISO 9001-2008 & 14001 : 2004 kupata cheti cha
Serikali ya India,chini ya Wizara ya Maendeleo ya Rasilimali Watu ya Serikali
ya India.Taasisi hii inatumika kuitangaza Elimu ya India kimataifa na
kuwadahili wanafunzi katika vyuo na taasisi zilizopo India.
Post a Comment