Ads

NAPE NNAUYE NA NAIBU WAKE ANNASTAZIA WAMBURA WAKARIBISHWA WIZARANI

Na John luhende
Mwamba wa habari blog
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mh,Nape Nnauye [ katikat]i ,kulia ni Naibu waziri wake Mh,Annastazia Wambura [aliyesimama] ni Olegabriel Elisante Katibu Mkuu wa wizara hiyo, akiwakaribisha wizarani hapo.[Picha na John Luhende ]Add caption



Wafanyakazi wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo,  wametakiwa kuwa na nidhamu na kuheshimiana kwa wakubwa na wadogo,mfanyakazi wa chini hadi ngazi za juu ili kuleta ufanisi na kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano.

Hayo yamesemwa na Waziri wa wizara hiyo Nape Nnauye wakati akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo makao makuu katika hafla ya kumkaribisha ofisini kwake baada ya kuteuliwa na rais Dk. M agufuli na kuwaomba watumishi wote kumpa ushirikiano yeye pamoja na Naibu wake.

Aidha Nape amesema kuwa wizara hiyo imekuwa ikipatiwa bajeti ndogo ukilinganisha na ukubwa wa majukumu yake na amehaidi kuipigania bajeti hiyo iongezwe ili iweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo.


Pamoja na hayo ameongeza kuwa atakuwa karibu na waandishi wa habri pamoja na wamiliki wa vyombo vya  habari na amesema  atakuwa mlezi badala ya mtawala ili kutatua changamoto ziizopo.

Viongozi na Wafanyakazi wa Wizara pamoja na Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Habar hayupo pichani.











Katibu Mkuu wa wizara hiyo Olegabriel Elisante akiwakaribsha waziri na Naibu katika ofisi za wizara hiyo.



Waziri akisisitiza jambo.
Picha zote na John Luhende  

No comments