Wizara ya nishati na madini yazindua mfumo mpya wa malipo ya leseni za madini
Kamishna msaidizi wa madini kitengo cha leseni John Nayopa Akizungumza na waandishi wa habari.picha na John Luhende. |
Na Jesca Mathew
mwambawahabariblog
Wizara ya nishati
na madini imezindua mfumo wa malipo ya ada za leseni za madini kwa njia ya
mtandao kupitia mfumo wa kielektroniki ujulikanao kama Online Mining Cadastre
Transaction Portal [OMCTP] ambao utaanza kutumika kwa mfumo wa malipo kwa njia
ya mtandao kuanzia tarehe 10 Desemba
2015.
- Akizungumza na waandishi wa habari Kamishna Msaidizi wa madini kitengo cha Leseni Bwana John Nayopa amesema kuwa mfumo huo utaweza kupunguza tatizo la mlundikano wa maombi ya leseni za madini kwenye ofisi za madini pamoja na kuongeza uwazi na kasi ya utoaji wa eseni za madini
Aidha
amesema kuwa mfumo huu ni rahisi Zaidi na wa haraka hivyo amewataka wachimbaji
wadogo wadogo kutumia mfumo huo ili waweze kupata huduma kwa wakati kwa kuwa
mfumo huu utahusisha mitandao ya simu.
Bw. Nayopa
ameongeza kuwa hadi sasa leseni 5919
zimesajiliwa ambapo pia kuna maombi 117 na
leseni za utafutaji leseni za uchimbaji mkubwa na wa kati zilizosajiliwa ni 111 pamoja na leseni hai za uchimbaji mdogo
zilizosajiliwa kwenye huduma hiyo ni 2,593 huku
jumla ya kampuni hai 370 zimesajiliwa.
Hata hivyo
wizara inawakumbusha wateja wote kuwa ili kujisajili kwenye mfumo huo wa OMCTP wanatakiwa
kuwasilisha nyaraka zifuatazo;
Fomu ya
kuomba usajili wa OMCPT iliyojazwa kikamilifu.
Leseni
halisi pamoja na stakabadhi za malipo ya leseni husika kutokea leseni husika
ilipohusishwa kwa mara ya mwisho hadi wakati wa kuomba usajili.
Kushoto ni Mkurugenzi msaidizi wa habari maelezo Vicent Tiganya.Picha na John Luhende |
Post a Comment