MKUU WA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE ATEMBELEA SABASABA
MKUU wa Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere(MNMA) ,Prof.Haruni Mapesa ametembele Banda la Chuo katika Maonesho ya 49 Kimataifa ya Biashara(SABASABA) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius K.Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Prof.Mapesa ametembelea Leo Julai 3,2025 na pia ametumia nafasi hiyo kuwakaribisha watanzania kujitokeza kwa wingi kutembelea Banda lao ili kupata historia ya chuo na kujionea bunifu mbalimbali zinazofanywa na wanafunzi.
Aidha ,amesema Chuo cha MNMA kinahistoria ndefu kilianzishwa na Mwalimu Nyerere mwezi Julai 29, 1961 miezi michache kabla yakupata uhuru.
Pia ameeleza kwamba Chuo kilianzishwa kwa lengo la kuandaa viongozi wa Tanzania ambao wameongoza baada yakupata uhuru.
"Chuo hiki kimepewa jina la Mwalimu Nyerere kwa ajili ya kumuenzi mwalimu kwa juhudi kubwa yakuwaelimisha watanzania lakini pia kuokoa nchi ya Tanzania",alisema
Hata hivyo, amesema kuwa Chuo kina majukumu matatu makubwa yakutoa elimu yaani mafunzo kwa wataalam kwa kuanzia ngazi ya wataalamu wa cheti hadi shahada za Umahiri.
Sanjari na hayo Prof.Mapesa amesema kwamba Chuo kina jukumu lakufanya utafiti na kutoa machapisho mbalimbali yanayohusu utafiti huo.
Profesa Mapesa pia amewakaribisha vijana wanaojiandaa kujiunga na chuo kutembelea Banda Hilo kwani wataweza kupata nafasi yakujiandikisha hapo hapo na kupewa usajili.
Aliendelea kwamba hiki ni chuo kinachotunza historia ya nchi na wao wamejipanga vizuri kuwaelimisha watanzania kwa weledi.
Post a Comment