Ads

KKKT YAKEMEA MAUAJI NA UTEKAJI NCHINI ,WAKIMZIKA ASKOFU SENDORO

 

 Umoja Wa Vijana KKKT Kawe - Dhambi nyingi za watu ni kwa ajili ya kufurahisha watu badala ya Mungu - DOKTA ALEX MALASUSA °Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani DOKTA ALEX MALASUSA amesema kuwa dhambi nyingi zimekuwa zikifanyika kwa sababu ya watu wengi wanapenda kufanya mambo yao kwa ajili ya kuwafurahisha watu badala ya Mungu. °Akihubiri katika Ibada ya Ijumaa Kuu Kanisa Kuu Azania Front DOKTA MALASUSA amesema kuwa Pilato alikubali Yesu asulubiwe na kumwachia mhalifu Baraba kwa sababu tu ya kutaka kuwafurahisha watu waliokuwa wakimshatiki. °Amesema katika Imani ya Kikristo jambo namba moja ni kumfurahisha Mungu kwanza na siyo watu. Askofu DOKTA MALASUSA pia amewaambia Wakristo kuwa mambo ya IMANI hayana kura kama ambavyo Wayahudi walipiga kura BARABA afunguliwe na YESU asulubiwe. #Soc,Upendo-Media | Facebook

 Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dk Alex Malasusa ametumia ibada ya maziko ya aliyekuwa Askofu wa Dayosisi ya Mwanga ya Kanisa hilo, Chediel Sendoro kukemea matukio ya utekaji na mauaji yanayoendelea nchini na kuiomba Serikali kuruhusu meza ya majadiliano.

Dk Malasusa amezungumza hayo leo Septemba 17, 2024 wakati akitoa salamu za kanisa katika ibada hiyo, iliyofanyika katika Kanisa Kuu Mwanga, mkoani Kilimanjaro, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini na Serikali akiwemo Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko.

Askofu Sendoro alifariki dunia Septemba 9, 2024 kwa ajali iliyotokea katika eneo la Kisangiro, Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro saa 1:30 usiku, baada ya gari alilokuwa akiendesha aina ya Toyota Prado, akitokea Kileo kuelekea nyumbani Mwanga, kugongana uso kwa uso na lori.

Akitoa salamu za Serikali, Dk Biteko amesema suala la utekaji na mauaji yanayoendelea nchini, tayari Rais Samia Suluhu Hassan alishatoa maelekezo ya uchunguzi kufanyika kwa haraka.

No comments