VETA YAPATA MWAROBAINI WA USIKIVU HAFIFU ,KUPIGWA PESA SASA BASI
Mwamba wa habari
Imeelezwa kuwa Kubuniwa kwa
kifaa cha usikivu hapa nchini huenda
watu wenye changamoto ya usikivu wakapata mkombozi atakaye wasaidia katika
changamoto hiyo.
Akizungumza na Mwamba wa
habari leo Julai 1-2024 katika banda la
VETA katika maonesho ya 48 ya biashara ya kimataifa mbunifu wa kifaa hicho mwalimu Innocent
Maziku, amesema changamoto ya usikivu aliyokuwa akipambana nayo ndiyo
ilimsukuma kutafuta suluhisho lake.
Maziku ambaye ni Mwalimu wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta) Kigoma amesema kifaa hicho kinauwezo wa kuwasaidia watu wenye changamoto ya usikivu hafifi na wakasikia vizuri.
Ameeleza kuwa huenda kubuniwa kwa kifaa hicho kutashusha gharama za ununuzi ambazo watu
wenye changamoto hiyo walikuwa wakizipata katika kununua vifaa kutoka Shilingi 500,000 kwa kifaa cha sikio moja cha analogia
na Shilingi milioni 1.2 kwa kifaa cha
kidigiti.
Akielezea kwa hisia na furaha aliyo nayo baada
ya kuona mafanikio makubwa ya chombo hicho Maziku amesema .
“Nilipata
changamoto hii ghafla alipokuwa darasa la sita, ikanifanya kupata shida shuleni masomoni na kifaa nicho nunuliwa kilishindwa kuni Saidia’’
Amesema
Post a Comment