Ads

WAZAZI CCM ILALA ILIVYOJIPANGA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANAFUNZI NA WALIMU

 
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala, Mhe. Mtiti Jirabi akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Msingi Olympio, wakati  akiwa katika ziara leo tarehe 9/3/2023.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala Mhe. Mtiti Jirabi (kushoto) akizungumza jambo na viongozi wa Kamati ya Shule ya Msingi Olympio, wakati akiwa katika ziara ya Shule hiyo leo tarehe 9/3/2023.

Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala Mhe. Mtiti Jirabi akipokea taarifa ya utendaji wa Shule ya Msingi Olympio kutoka kwa Mwenyekiti wa kamati ya Shule hiyo. Bw. Rajabu Amry,

Mwenyekiti wa kamati ya Shule ya Msingi Olympio Bw. Rajabu Amry akifafanua jambo katika kikao kazi na Kamati ya Utekelezaji wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Ilala.
Mkuu wa Shule ya Msingi Olympio Shule Bw. Reben Gadi (kutoka kushoto), Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Ilala, Mhe. Mtiti Jirabi, Diwani wa Kata ya Upanga Mashariki wakizungumza Jambo.

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Olympio iliyopo Kata ya Upanga Mashariki, Dar es Salaam wakiimba nyimbo ya Taifa.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala Mhe. Mohamed Msofe akizungumza jambo.

NA NOEL RUKANUGA, DAR ES SALAAM.
Kamati ya Utekelezaji wa Jumuiya ya Wazazi Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala leo tarehe 9/3/2023 imefanya ziara katika Shule ya Msingi Olympio kwa ajili ya kuzungumza na wanafunzi pamoja na kufanya kikao kazi na kamati ya Shule kwa ajili ya kujadili maendeleo pamoja na kuangalia namna ya kutatu changamoto zilizopo kadri inavyowezekana.

Kamati hiyo ya utekelezaji inasimamiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Ilala Mhe. Mohamed Msofe na Katibu wa Wazazi CCM Wilaya ya Ilala Mhe. Mtiti Jirabi akiwa mtendaji mkuu,  ambapo lengo ni kutembelea shule zote za msingi na sekondari zilizopo Wilaya ya Ilala kwa ajili ya kuangalia utekelezaji majukumu ya uongozi wa shule pamoja na  kuhakikisha watoto waansoma katika mazingira rafiki.

Akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Msingi Olympio Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Ilala, Mhe. Mtiti Jirabi amewataka wanafunzi kuwa na nidhamu jambo ambalo litawasaidia kuishi vizuri katika maisha yao na kupiga hatua katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo.


Mhe. Jirabi amebainisha kuwa kuna wimbi kubwa limejitokeza la ubakaji wa watoto, hivyo amewasihi wanafunzi kuishi na kukaa na wazazi wao vizuri pamoja kutii maelekezo yao.

“Tuepuke na vitendo ambayo sio rafiki katika jamii, kwani Taifa linawategemea, waziri atatokea hapa, Rais atatokea hapa, viongozi watatokea hapa someni kwa bidii” amesema Mhe. Jirabi.

Katibu huyo ametumia fursa hiyo kueleza majukumu ya Jumuiya ya Wazazi Chama Cha CCM .

Mwenyekiti wa kamati ya Shule ya Msingi Olympio Bw. Rajabu Amry, amesema kuwa kutokana na mazingira ya shule watoto wanatoka mbali kuja kusoma katika shule hiyo.

Bw. Amry amesema kuwa changamoto iliyopo watoto wanaishi mbali na shule na kusababisha kuchelewa kufika shule kwa ajili ya kuendelea na masomo.

“Hatuna gari la shule kwa ajili ya usafiri wa wanafunzi, usafiri wanaotumia kwa sasa sio rasmi” amesema Bw. Amry.

Mkuu wa Shule ya Msingi Olympio Shule Bw. Reben Gadi, amesema kuwa pia kuna changamoto  ukosefu wa madarasa kwani kwa sasa kuna madarasa 25.

Amesema katika jitihada za kukabiliana na changamoto hiyo wamefanikiwa kuanzisha mradi wa ujenzi wa gorofa nne katika shule hiyo.

“Katika gorofa nne kutakuwa madarasa 11, ofisi tano, chumba cha huduma ya kwanza, chumba cha kuifadhia vitu, kumbi za mikutano, Maktaba moja pamoja na  matundu ya vyoo 64.

Kamati ya Utekelezaji wa Jumuiya ya Wazazi Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala inatarajia kuendelea na ziara tarehe 10/3/2023 katika shule ya Sekondari Jamhuri.

No comments