Ads

MSANII WA REGGAE KUTOKA NEW YORK KUTUA TANZANIA KUTAMBULISHA ALBUM YA 'SIDE OF THE TIME'

Msanii wa muziki wa Reggae kutoka New York nchini Marekani Nat Sterling ambaye ametoa album yake inayojulikana kwa jina la  'Side of the time’ yenye nyimbo 12 ambazo  zimebeba maudhui ya wapendanao yenye lengo ya kuelimisha jamii kuhusu maana ya siku ya wapendanao.

NA NOEL RUKANUGA, DAR ES SALAAM

Msanii wa Muziki wa Reggae kutoka New York nchini Marekani Nat Sterling anatarajia kuja nchini Tanzania kwa ajili kufanya ziara pamoja kutambulisha album yake mpya inayojulikana kwa jina la 'Side of the time'  kupitia maonesho mbalimbali anayotarajia kufanya.

Katika album ya 'Side of the time’ ina nyimbo 12 ambazo  zimebeba maudhui ya wapendanao yenye lengo ya kuelimisha jamii kuhusu maana ya siku ya wapendanao kwani baadhi ya watu wengi duniani wanatafsiri siku hiyo tofauti.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mratibu wa ziara ya Msanii Nat Sterling, Bw  Dimateo Zion, amesema kuwa maandalizi ya msanii huyo wa Reggae kutoka New York nchini Marekani kuja Tanzania yanaendelea vizuri  na anatarajia kuwasili hivi karibuni.

Zion amesema kuwa lengo ya ziara ni kutambulisha album yake kwa wadau wa nyimbo za reggae pamoja na kuhakikisha wanashirikiana na wasanii wengine hapa nchini katika kuhakikisha kwa namna moja au nyengine mziki wa Reggae unasonga mbele.

"Anatarajia kutambulisha nyimbo 12 kupitia maonesho  mbalimbali atakayofanya, tunawaomba watanzania kutoa ushirikiano kwa msanii huyo wa Kimataifa kutoka New York, Marekani" amesema Zion.

Katika album yake ya  “Side of the time” kuna nyimbo 12 ambazo ni Phantom, Viper, Moon light, Rasta shines, Nice, You make me smile, Rock my world, Young Lady, Woman it's you, Your love, sign of the time pamoja na Where is the love.

No comments