Ads

MIPANGO CHAONGEZA KOZI MPYA

 



Na. Wellu Mtaki , Dodoma.

Katika kuhakikisha  kunakuwepo na wigo mpana wa ajira Chuo cha mipango ya maendeleo vijijini chaongeza cha Jijini  Dodoma kimeanzisha  kozi mpya  za tehama, upimaji ardhi  pamoja na uhasibu na fedha. 

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Baraza la uongozi wa chuo cha mipango ya maendeleo vijijini prof Martha Qorra wakati akizungumza na wahandishi wa habari jijini dodoma katika  ufunguzi wa kongamano la kufanya mapitio ya baadhi ya mitaala ya zamani na mitaala mipya ambayo inaanzishwa chuoni hapo.

Naye mkuu wa chuo hicho  prof Huzen Mayaya ,amesema kozi zinazotolewa na chuo hicho cha serikali  ni bora na zinakwenda kuwasaidia wahitimu wengi kupata zana ya kujiajiri wenyewe.

Kwa upande wake makamu mkuu wa chuo cha mipango ya maendeleo vijijini anayeshughurika na taaluma , utafiti na ushauri  prof provident Dimoso amesema chuo kinajikita katika utoaji wa elimu Kwa vitendo  ili kusaidia wimbi la wahitimu kujiamini na kuelewa zaidi hata waendapo mitaani waweze kujiajiri na kuwa na sifa za  kuajiriwa. 

Chuo cha mipango ya maendeleo vijijini ni chuo kilichoanzishwa KWa lengo la kusaidia vijana baada ya kufanyika utafiti  kugundulika ipo haja ya vijana kuwa na mipango ambao hitawaaaidia katika maisha yao.


No comments