TRA YAJIPANGA KUKUSANYA TRILIONI 23.65 MWAKA WA FEDHA 2022/ 2023
Mkurugenzi wa
Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard
Kayombo akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 12.8.2022 jijini Dar es
Salaam kuhusu mkakati wa makusanyo ya kodi mwaka 2022/2023.
NA NOEL RUKANUGA, DAR ES SALAAM.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inatarajia
kukusanya Shilingi Trilioni 23.65, ikiwa ni sehemu ya bajeti kuu ya Serikali ya
Shilingi Trilioni 41.48, huku mwaka wa fedha 2021/2022, walifanikiwa walikusanya kiasi cha shilingi Trilioni 22.99.
Akizungumza na waandishi wa
habari leo tarehe 12.8.2022 jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Huduma na Elimu
kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo, amesema
kuwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 wanatarajia kukusanya Shilingi Trilioni 23.65,
ikiwa ni sehemu ya bajeti kuu ya Serikali ya Shilingi Trilioni 41.48.
Bw. Kayombo amesema kuwa ongezeko
hilo linatokana na kuendelea kutoa elimu
ya ulipaji kodi kwa wafanyakazi na wafanyabiashara kuhusu sheria za kodi, tozo
na ada zilizofanyiwa marekebisho ili kuhakikisha wanakuwa na uelewa sawa na
kurahisisha ukusanyaji na ulipaji kodi kwa hiari.
Amesema kuwa kwa sasa watanzania
wanatakiwa kuendelea kulipa kodi kwa hiari ili kufanikisha utekelezaji wa bajeti
ya Serikali ya mwaka wa fedha 2022/2023.
“Tumeanza kuelimisha umma kuhusu mabadiliko
ya sheria mbalimbali za kodi, tozo na ada zinazosimamiwa na TRA pamoja na
taratibu za ukusanyaji na usimamiaji wa mapato ya Serikali jambo ambalo
linaleta tija katika kukusanya kodi.” amesema Bw. Kayombo.
Amesema kuwa marekebisho na mabadiliko ya sheria za kodi yamefanyika kwa
lengo la kuongeza kasi ya kufufua uchumi na kuimarisha sekta za uzalishaji kwa
ajili ya kuboresha maisha ya wananchi.
Bw. Kayombo ameeleza kuwa miongoni
mwa mabadiliko ni pamoja na sheria ya usimamizi wa kodi ambayo inamtaka kila
mwananchi mwenye Namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) kupata Namba ya
Utambulisho wa Mlipakodi (TIN).
Amefafanua kuwa mabadiliko ya sheria ya usimamizi wa kodi, Sheria ya sasa
inamtaka kila mwananchi mwenye namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA)
kusajiliwa na kupata namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN) ili kumwezesha
katika kufanya shughuli za kiuchumi.
“Mwaka wa fedha 2021/2022, TRA ilifanikiwa kutatua changamoto za
walipakodi, kuweka mazingira mazuri ya kulipa kodi, kuongeza kasi ya kusajili
walipakodi wapya, kuwekeza kwenye TEHAMA na kutoa elimu na kuhamasisha” amesema
Bw. Kayombo.
Katika kuhakikisha TRA inaendelea kufanya kazi kwa ufanisi wameendelea kutoa elimu katika jamii kwa nyakati tofauti ikiwemo kwa wafanyabiashara wadogo na wakubwa ili waweze kufikia malengo tarajiwa.
Post a Comment