WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII ATOA AGIZO LA MIKOA YOTE KUIGA MFANO WA MKOA WA SHINYANGA
WAZIRI
WA MALIASILI NA UTALII ATOA AGIZO LA MIKOA YOTE KUIGA MFANO WA MKOA WA
SHINYANGA KATIKA KUJENGA VIJIJI VYA MAONYESHO YA UTAMADUNI KWA AJILI YA
MAKABILA YAO
Agizo
hilo limetolewa siku ya Leo na Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa
Pindi Chana wakati alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri Mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye ufunguzi wa Kijiji Cha Utamaduni
kilichofanyika katika Mkoa wa Shinyanga
Ambapo
Mheshimiwa Waziri amesema anamshukuru Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga
Mheshimiwa Sophia Mjema kwa ubunifu mkubwa alioufanya wa kutii na
kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia
Suluhu Hassan la kuhakikisha kila Mkoa unaenzi na kudumisha tamaduni zao
hivyo Mkuu wa mkoa akaamuwa kufanya ubunifu mkubwa wa kuhakikisha
amejenga Kijiji ambacho kitakuwa ni maalumu katika kuenzi na kudumisha
utamaduni wa makabila yote yaliyopo katika Mkoa huo yanadumishwa na
kuenziwa vizuri
Aidha
Mheshimiwa Pindi Chana ametoa wito kwa Mikoa yote nchini kuiga mfano
uliofanywa na Mkoa wa Shinyanga katika kujenga vijiji na kuenzi makabila
na tamaduni zao zote hivyo akatoa msisitizo wa jambo Hili kuhakikisha
Mikoa yote imefanya na kuhakikisha inadumisha vyema tamaduni na kabila
zote zilizopo katika Mikoa
'Natoa
agizo kwa Mikoa yote nchini kuhakikisha inaiga mfano huu ambao
umeandaliwa na Mkoa wa Shinyanga ni ubunifu mzuri mno ambao tumejionea
ni kwa namna gani Machief na watemi zamani walivyokuwa wakiishi na
maisha yao halisi pia mpangilio mzuri wa Kijiji kimoja ambacho kimekuwa
na maonyesho ya tamaduni kwa wilaya zote zilizopo katika Mkoa huu hivyo
nahitaji Mikoa mingine yote ifanye ubunifu huu ili tuweze kuona makabila
yao na tamaduni zao zikienziwa na hili ndilo agizo la Mheshimiwa Rais
wetu' amesema Waziri
Sambamba
na ufunguzi huo wa Kijiji Cha Utamaduni kwa Mkoa wa Shinyanga
Mheshimiwa Waziri alizindua pia filamu ya Royal Tour kwa Mkoa wa
Shinyanga iliyochezwa na Rais wa Jamhuri wa Tanzania Mama Samia Suluhu
yenye lengo la kutangaza Vivutio vya Utalii vilivyopo nchini pamoja na
kuitangaza Tanzania kimataifa zaidi
Kwa
upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Sophia Mjema amesema
anajivunia na anaona ufahari mkubwa kwa jinsi na namna machief na watemi
katika Mkoa huo walivyojitoa katika kuhakikisha wanafanikisha vyema
zoezi Zima la kuonyesha utamaduni kwa Mkoa linafanikiwa vyema
Aidha
ameongeza kwa kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama
Samia kwa jinsi anavyoipeperusha vyema Bendera ya Tanzania katika
kuhakikisha kila mwananchi anafurahia matunda ya Nchi yake sambamba na
kuitangaza nchi kimataifa.
Post a Comment