Ads

DC LUBIGIJA AKUTANA NA WATENDAJI SERIKALI ZA MTAA KUTATUA CHANGAMOTO SEKTA YA ARIDHI.


Na Francisco Peter, Dar es Salaam

Mkuu wa wilaya ya Ilala Bwilaguzu Lubigija ameyataka Makapuni ya Urasmishaji wa Ardhi kutekeleza Majukumu yao kwa weledi.

Akizungumza katika kikao Cha Wenyeviti wa Serikali za mitaa na Watendaji wa Ardhi jijini Dar es Salaam Bwilaguzu Lubigija amesema wale watakao bainika makampuni yao hayatafanya kazi kwa weledi watachukuliwa hatua.

"Kampuni zinazolalamikiwa nazitaka kuja kwenye kikao Jumanne ijayo watakaoshindwa nitatumia nguvu zaidi kuwapata". amesema Lubigija.

Lubigija amesema ili wananchi waweze kutumia hati zao kuweza kupata mikopo katika taasisi za kibenki.

Aliongeza kampuni za kihuni zilizochukua fedha  na kushindwa kufanya kazi zitachukuliwa hatua za kisheria.

"Katika zoezi hilo la  Urasmishaji linatupelekea katika kupata hati". alisisitiza.

Ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kushiriki zoezi la urasmishaji wa ardhi katika maeneo yao.

Kaimu Kamishina wa Ardhi wa Mkoa wa Dar es Salaam Idrisa kayela, ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kushiriki zoezi la urasmishaji wa ardhi katika maeneo yao na amesema jumla ya viwanja 2,28000 vimetambuliwa kati viwanja 6000,00 na hati 4000 zimetambuliwa.

"Mikakati ni kumilikisha mitaa hati 105 ambapo kumekuwa na ushirikishwaji mdogo". Amesema  kayela.

Kayela amesema kuwa kumekuwa na changamoto ya baadhi ya watalamu ambapo kumekuwa na maeneo yamepimwa lakini kumekuwa natatizo la uthibitisho wa umililiki wa ardhi.

Aliongeza kuwa kumekuwa changamoto ya Elimu na uhudhuriaji wa Mafunzo ya Urasmishaji.

"Zoezi hili lilianza Mwaka 2013 linatarajiwa kumalizika 2025 kwasasa Gharama imeshuka kutoka shilingi 150000 Hadi kufikikia shilingi 130,000'". Alisisitiza Kayela.

Kayela alibainisha kiasi kilichokusanywa nishilingi bilioni 22 huku lengo likiwa ni bilioni 79.

No comments