TARURA WAONDOLEWA KUKUSANYA USHURU WA MAEGESHO.
Na,
Vestina Mlandali, Dar es Salaam.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Innocent Bashungwa
ameagiza kazi ya kukusanya ushuru wa maegesho ya magari, iliyokua chini ya
Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura) irudishwe kwenye Mamlaka za
Serikali za Mitaa.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Waziri Bashungwa ametoa maagizo hayo hapo Jana wakati wa Kikao chake na Uongozi wa Tarura na
mawakala wa ukusanyaji ushuru wa maegesho kwenye halmashauri mbalimbali nchini.
Amesema
kuwa, naona malalamiko kutoka kwa wananchi hayaishi kuhusiana na chanzo
hiki na Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan hafurahishwi na malalamiko
haya ya wananchi kila mara na kuwataka Tarura wazidi kufanya Kazi Yao kiumahili
zaidi.
Pia
ameeleza kuwa, hili la ukusanyaji wa parking sio jukumu la msingi la Tarura,
hivyo nalirudisha halmashauri, ili ninyi Tarura mkasimamie kutengeneza barabara
na miundombinu mbalimbali katika jamii.
"Nataka
kuazia Sasa Tarura iweze kufanya Kazi yake Kwa umahili wa Hali ya juu sitaki
Tena wananchi walete malalamiko kuhusu suala nzima la miundo mbinu hivyo nataka
halmashauri iweze kusimamia vinzuri suala nzima la ushuru na Tarura ifanye Kazi
ya miundo mbinu tu". Amesema
Pia
amemuelekeza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Prof. Riziki Shemdoe kusimamia
makabidhiano ya chanzo hicho haraka baina ya Tarura na Mamlaka za Serikali za
Mitaa
Ameongeza
kuwa: “Nitapenda kuona sasa Tarura mkielekeza nguvu kwenye kuimairisha
miundombinu ya barabara za mijini na vijijini na mkafungue barabara na kufika
kusikofikika, madaraja yakajengwe, makalavati ili kurahisha usafiri kwa
wanannchi wetu,” amesema.
Post a Comment