KAMPUNI YA SUKARI YA KILOMBERO ILIVYOJIPANGA KUDHIBITI KUPANDA KWA BEI YA SUKARI KIPINDI CHA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI.
.......
Kampuni ya Sukari
Kilombero imewasihi Wafanyabiashara wote wa jumla na rejareja wanaouza bidhaa
za "Bwana Sukari kutokupandisha bei kuelekea mfungo wa ramadhani
unaotarajiwa kuanza mwanzo mwa mwezi aprili mwaka huu ili kusaidia kuepuka
taharuki inayoweza kujitokeza kwenye kipindi Cha mfungo wa Mwezi Mtukufu wa
ramadhani.
Tamko hilo limetolewa
Jijini Dar es salaam na Mkuu wa idara ya biashara wa kampuni ya Sukari
kilombero Bw.Fimbo Butallah wakati akizungumza na wanahabari kutokana na
historia yakupanda kwa bei ya bidhaa za vyakula kila uanzapo mfungo wa mwezi
Mtukufu wa ramadhani nakusababisha adha kubwa kwa waumini wanaofunga mwezi huo.
Butallah amesema
katika uchumi wa soko huria wao Kama wazalishaji hawaruhusiwi kuwapangia
Wafanyabiashara bei yakuuza bidhaa lakini wanawajibu mkubwa wakuwashauri
upandishaji holela wa bei hasa pale ambapo wazalishaji hawajapandisha bei ya
bidhaa hiyo.
"Tunawasihi
Wafanyabiashara kote Nchini kutopandisha bei ya Sukari katika Mwezi Mtukufu wa
ramadhani ili kuepuka taharuki inayoweza kujitokeza " amesema kuu huyo wa
idara ya biashara wa kampuni ya Sukari Kilombero.
Bw.Butallah amendelea
kusema kuwa suala la uhaba wa Sukari ambalo Mara nyingi limekuwa likijitokeza
kwenye mfungo wa ramadhani Kampuni ya Sukari Kilombero inayo akiba yakutosha
kulivusha Taifa katika mfungo huo Mtukufu nakuongezea ,ambapo tayari kampuni
imepata kibali chakuagiza Sukari kutoka nje ya Nchi kuziba pengo la uzalishaji.
Kampuni ya Sukari ya
Kilombero ambayo inamilikiwa na Kampuni ya An illovo Sugar Africa kwa asilimia
75 na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 25, ipo katika
maandalizi ya Mradi wake wa upanuzi ambao utakuza uwezo wa kampuni hiyo wa
kuzalisha Sukari na kupunguza uhaba wa Sukari Nchini kupitia chapa yake ya
"Bwana Sukari.
Post a Comment