MWENYEKITI MTAA WA ULONGONI AFUNGUKA MIPANGO UTEKELEZAJI UJENZI WA OFISI
Mwenyekiti wa Serikali za
Mtaa Kata ya Ulongoni (A), Ukonga jiji la Ilala, Bw. Abdulrahm Munisi
akizungumza jambo na waandishi wa habari katika Mkoa wa Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu, Dar es
Salaam.
Mwenyekiti
wa Serikali za Mtaa Kata ya Ulongoni (A), Ukonga jiji la Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Abdulrahm Munisi amesema
kupitia uongozi wake amefanikiwa kutekeleza majukumu yake kwa kupambana
changamoto zilizopo kwenye kata hiyo.
Mwenyekiti huyo ambaye
hadi hivi sasa ana miaka miwili kwenye uongozi na tayari ameanza ujenzi wa
ofisi ya kata na kwa sasa wanafanya shughuli zao kwenye ofisi ya kupanga.
Akizungumzia ujenzi wa ofisi
ya kata Bw. Abdulrahm Munisi amesema kuwa ofisi hiyo ina unachumba cha ukumbi
na ofisi ya mtendaji ambayo inastoo
ndogo.
"Kata
yetu hii ina muda mrefu tangu 2009 haijaweza kuwa na Ofisi yake, hivyo naitaji
kukamilisha ujenzi ili kata iweze na ofisi yake," amesema Munisi.
Amesema kuwa kupitia mradi
wa songasi kuwepo katika kata hiyo, ndicho kimekuwa chanzo cha kupata pesa
kidogo wanazolipwa kutokana na kata hiyo, kuwa walinzi wa mradi huo.
Amesema
kuwa wanaunga mkono juhudi za serikali kwa kuweza kuwajenga madarasa mawili ya
shule ya msingi Ulongoni A, ambapo januari 17 wameanza kutumika baada ya shule
zote nchini kufunguliwa.
Amefafanua kuwa kutokana na kata hiyo haina chanzo kingine cha mapato wamemkumbusha Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Bw. Jumanne Shauri kwani mwa mwaka jana walimwandikia barua.
katika kuendeleza
maendeleo ya Ulongoni A eneo inapojengwa ofisi hiyo inayoitaji mwendelezo
kukamilika lilitolewa na mkazi wa eneo hilo mwaka 2009.
Uongozi wa kata hiyo kupitia kwa Mtendaji kata Jenifa Shayo wametaja kukamilika kwa majukumu mbalimbali kwa kupambana na utatuzi wa changamoto wanazokuwa nazo wananchi.
Post a Comment