Ads

UKWELI KUHUSU CHANZO CHA UGONJWA WA KIFAFA.

 

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya kifafa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Patience Luoga akitoa ufafanuzi kuhusu ugonjwa wa kifafa.

Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam.

Imeelezwa kuwa baadhi ya wagonjwa wa kifafa hutokana na ajali hivyo waendesha boda boda nchini wametakiwa kuwa makini kipindi wanapokuwa wanaendesha Ili kuzuia ajali za mara kwa mara barabarani

Hayo yamesemwa Dkt. Bingwa wa Magonjwa ya kifafa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Patience Luoga, amesema  katika hali hiyo kifafa kinasababishwa na degedege ambapo wagonjwa wenge wametajwa kuanzia umri wa wastani miaka 15 na zaidi ya asilimia 25 ya wagonjwa wa kifafa Wana ulemavi .

"Hali ya ulemavu huo husababishwa na kuanguka wakati wa ugonjwa anapopata degedege na nchini Tanzania zaidi ya watu milioni moja  wanaugonjwa wa kifafa,"anasema Dkt Luoga.

Dkt. Luoga amesema kwa kuwa watajwa hapo wengi ni wenye wastani miaka 15 ndio hasa takwimu zinaonesha hivyo na kwakua  boda boda wengi ni vijana na amewaasa kujilinda kutokupata ajali za barabarani ilikuja kuepukana na matatizo ya kupata kifafa pindi wapatapo ajari.

Aidha amesema visa vya bodaboda ni vingi vya wanaofika kupatiwa matibabu katika Hospitali hiyo  ya Taifa ya Muhimbili .

Aliendelea kueleza kuwa watu wanaoishi na kifafa no zaidi ya watu 60 milioni Duniani kote na niongezeko la watu 34 Hadi 76 kwa watu 200000 kwa mwaka.

Serikali kutoa elimu vijijini na utoaji dawa za kutosha kutibu wagonjwa hao , hali inayoweza kupunguza kiwango cha ugonjwa wa kifafa huku zaidi ya asilimia 25 ya wagonjwa wa kifafa wakitajwa  wanaulemavu  unaosababishwa na kuanguka wakati wa ugonjwa kutokana na kupata degedege.

Madaktari wa Muhimbili wataadhimisha siku hiyo ambayo itafanyika Februari 14  mwaka huu  kwa kutoa elimu kwa jamii .

Chama Cha Wagonjwa wa Kifafa nchini (TEA), kuelekea siku hiyo kimeweza kuzunguza na wananchi kwa kutumia vyombo vya habari , kwamba ugonjwa huo unatibika na hivyo  kuacha imani za kishirikina na badala yake kimewataka kuwapeleka wagonjwa hospitali mapema.

“Wengi wana imani potofu kwamba mtu mwenye kifafa, kimesababishwa na mashetani, lakini si kweli kwani  wanasayansi walibaini kuwa mshutuko wa ubongo ndio unasababisha kifafa kutokana na sababu mbalimbali,” amesema Dkt.Luoga.

Hospitali ya Taifa Muhimbili mara zote imekuwa ikipambanua kua, mtu anapata kifafa wakati anapozaliwa endapo ataumia sehemu ya kichwani, kukosa hewa au mtoto kuumizwa kichwani kua atapata degedege.

No comments