AGIZO LA KATIBU MKUU WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUHUSU MATUMIZI YA FEDHA KUBORESHA KIJIJI CHA MAKUMBUSHO
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. France Michael amewaagiza watendakazi wa Makumbusho ya Taifa kuhakikisha kiasi cha fedha shilingi milioni miambili na moja zilizotengwa na Mhe Raisi Samia Suluhu za miradi zinatumika kwa mlengo uliokusudiwa.
Agizo hilo amelitoa leo
Jijini Dar es salaam katika Uzinduzi wa Uboreshaji wa Kijiji Cha Makumbusho
Kukuza Utalii wa Kiutamaduni kupitia mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na
mapambano dhidi ya Uvico 19 ambapo amesema fedha hizo zitasaidia kujenga nyumba
za asili ya makabila mbalimbali ikiwemo wazanaki ili kuendelea kulinda
utamaduni wao.
Sanjari na hayo Dkt. Michael
amesema fedha hizo zitajenga nyumba za asili za makabila mbalimbali ikiwemo
Wazanaki ili kusaidia kuhifadhi vitu vya asili na nyaraka zao na kuvutia
watalii ndani na nje na zitafanya
maboresho katika vituo vyote ili kusaidia kuvutia Utalii wa kiutamaduni na
kuongezeka watalii na watafiti kufanya
tafiti zao na itakua chachu kuvutia watalii wengi na pato la Taifa kuongezeka..
"Miradi hii imezinduliwa
kutokana na fedha hizo nakuwa ni matarajio zitakwenda kukuza utalii na
unategemea kubadirisha taswira ya makumbusho,"amesema Dkt. Michael.
Kwa upande wake Mkurugenzi
Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt. Noeli Luoga amemshukuru Raisi kwa jitihada
kubwa kusaidia kuboresha miundombinu na vituo vya utalii Nchini na kukuza
Uchumi wa Taifa
Post a Comment