Ads

TMDA YAANZA RASMI KUTOA ELIMU KUHUSU MATUMIZI YA BIDHAA ZA TUMBAKU.



Mkuu wa kitengo cha mawasiliano kwa umma wa Mamlaka ya dawa na vifaa tiba (TMDA) Gaudensia Simwanza akitoa huduma kwa mteja aliyefika katika banda la mamlaka hiyo.




Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya dawa na vifaa tiba (TMDA)  Bwana Adam  Fimbo,  wapili kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya dawa na vifaa tiba (TMDA) 

Mamlaka ya dawa na vifaa tiba (TMDA) imesema imeanza kuweka utaratibu na mfumo katika kudhibiti wa bidhaa za tumbaku.

Hayo yamebainishwa na mkurugenzi mkuu wa malaka hiyo Bwana Adam  Fimbo,  katika viwanja vya maonesho ya biashara ya kimataifa (Sabasaba ) wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda la mamlaka hiyo.

"Kuanzia mwezi wanne mwaka huu tumepewa kazi  ya kudhibiti bidhaa za tumbaku na waziri wa Afya ,sheria ilikuwepo tangu mwaka 2003 lakini  hapakuwepo na malaka rasmi ambayo iliundwa kwaajili ya kusimamia na kudhibiti bidahaa hiyo" Amesema 

Amesema kupitia sheria hiyo TMDA imejikita zaidi katika kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya tumbaku ambayo ni magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama  Kansa za koo,mapafu , shinikizo la damu magonjwa kwenye mfumo mzima wa Moyo na  damu .

Sheria hii pia inazuia watu wenye chini ya umri wa miaka 18 kuvuta sigara ,na pia tumbaku ambazo hazivutwi haziruhusiwi kutumika.

"Tutaendelea kuwapa elimu wale wote wananotumia tumbako  na kuvuta sigara ili waache taratibu nawale ambao hawajajiingiza katika matumizi ya tumbaku waache kabisa kutokana na madhara haya niliyo yaeleza  nikazi kubwa lakini tumejipanga kuitekeleza   kama tunavyo fanya katika dawa, vifaa tiba na vitendanishi"Amesema.

Sheria hii pia inaeleza kuhusu kutenga maeneo maalumu ya kuvuta sigara hasa maeneo yanayo husisha watu wengi ili moshi usiwafikie watu wengine ambao hawavuti.

"Meneo ya migahawa,baa na mikusanyiko mbalimbali inayoleta watu karibu inapaswa kuwa na maeno hayo ,mtu ambaye havuti sigara anapo puliziwa moshi na mvutaji anapatwa na madhara haya"Amesema.

Kwa maelzeo zaidi fika katika banda la TMDA  katika viwanja vya maonesho ukumbi wa Kilinjaro ili kupata elimu zaidi


No comments