Ads

Mkurugezi PBZ, huduma za bank ya watu wa zanzibar ni nafuu sana ,soma hapa kujua

 


Banda la Bank ya watu wa Zanzibar PBZ  lipo katika ukumbi wa Karume

Bank ya watu wa Zanzibar PBZ  imesema sababu ya watu wengi kuipenda Bank hiyo ni kutokana na huduma nzuri  zinazotolewa ikiwemo mikopo nafuu kwa wafanyakazi .

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi mwendeshaji wa Bank ya watu wa Zanzibar PBZ ,  Dakta Muhsin Salim Masoud  wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho ya 45 ya biashara ya kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Amesema Maonesho hayo yamesaidia Bank hiyo kujitangaza huduma zake kwa wananchi wanaotembelea  banda lao na watu wengi wameweza kufungua  Account ,na kupata kadi za VISA kwa haraka.

"Muonekano wa Bank ya PBZ   zamani ilikuwa inaonekana kama Bank ya Zanzibar Pekee wala siyo ya Tanzania Bara  lakini  hapa tumepata nafasi ya kuwa eleza kuwa Bank hii ni ya watu wote na imeenea sana Zanzibar na hapa bara "Alisema  

kumoja ya mafanikio yake makubwa n 'inawakaribimeishauri mamlaka ya maendeleo ya biashara Tanzania  

Bank  hii makao makuu yake  yako Zanzibar inayo matawi sehemu mbalimbali  matawi 16 bara na Zanzibar  tuna huduma za usafirishaji fedha nje ambazo ni zaharaka na kuaminika   ,tunatoa mikopo nafuu  kwa wafanyakazi wa serikali "Amesema

Pia amesema Bank  hiyo inampango wa kufungua matawi maeneo mbali mbali ikiwemo Tazara ,Lumumba ,kigamboni ,Tandika ,Arusha na Mwanza, Mtwara na karibuni litafunguliwa tawi jipya Tandahimba .

Aidha Dakta Muhsin  amesema,  Bank hiyo ina kitengo maalumu cha Bank ya kiislamu ambacho kinafanya miamala yake kwa kufuata sharia za kiislamu.

"Tofauti ya Bank  hii na Bank nyingine ni kwamba yenyewe haiuzi pesa kwa pesa ila ukitaka kuwezeshwa unawezeshwa kupitia vitu ,kwahiyo Bank inafanya biashara na wewe inachukua  risk  siyo ile bank ambayo inaacha risk zote kwa mteja "Amesema.


No comments