Ads

STAMICO YASHINDA MAONESHO SABASABA



Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeibuka kidedea kwa kuwa Mshindi wa kwanza kwenye Maonesho ya Sabasaba mwaka 2021.

Akiongea kwa furaha baada ya ushindi huo  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Dkt Venance Mwasse amesema STAMICO imekuja kivingine mwaka huu kwa kuja na Ubunifu mpya kwa  kwa kuleta bidhaa mpya katika soko kama vile Kiwanda cha Kusafisha Dhahabu, Mkaa Mbadala (Rafiki Briquettes) kwa ajili ya matumizi ya Nyumbani. Mafunzo kwa wachimbaji wenye usikivu hafifu (viziwi) ambao walipata Elimu kutoka STAMICO.

Ushindi huo umepatika baada ya kukidhi vigezo mbalimbali vya ushindi ikiwemo ubora wa banda (branding) Ubunifu, Huduma bora kwa wateja na utoaji bora wa elimu.




 

No comments