Ads

Kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) chatoa fursa kwa wananchi sabasaba.

 
Meneja uhamasishaji uwekezaji Kanda ya  Nyanda za juu kusini   wa kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC)  Bwana, Venance Mashiba akizungumza na wateja waliotembelea banda  hilo katika maonesho ya 45 ya biashara ya kimataifa  katika viwanja vya Mwalimu Julius  Nyerere (Sabasaba) Kilwa road jijini Dar es salaam.  



Afisa habari na  uhusiano wa  kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC)  Bi Robertha Makinda , akizungumza na wateja waliotembelea banda  hilo katika maonesho ya 45 ya biashara ya kimataifa  katika viwanja vya Mwalimu Julius  Nyerere (Sabasaba) Kilwa road jijini Dar es salaam.  


Kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) kinawakaribisha  wananchi  wote wanaotembelea maonesho ya 45 ya biashara ya kimataifa yanayo fanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius  Nyerere (Sabasaba) Kilwa road jijini Dar es salaam,  kutembelea banda  lake ili  waweze kujifunza mambo mbalimbali ikiwemo huduma zinazo tolewa .

Akizungumza na Waandishi wa habari , Meneja uhamasishaji uwekezaji Kanda ya  Nyanda za juu kusini  wa kituo hicho  Bwana, Venance Mashiba,  amesesema  kituo cha uwekezaji Tanzania kinashiriki maonesho hayo kwa lengo la kuufahamisha umma kuhusu shughuli za taasisi hiyo ambayo iko chini ya Serikali.

Amesema moja ya majukumu ya kituo  hicho ni kuhamasisha wawekezaji ,kuwasajili wawekezaji walio itikia wito wa kuwekeza ,katika makundi yote mawili  wawekezaji wa ndani na wanje.

Wawekezaji wa ndani husajiliwa kuanzia na mtaji wa Dolla 100,000.00 /= kwenye mradi  na wale wawekezaji wa nje husajiliwa kuanzia Mtaji wa Dolla 500,000.00/= na baadaye huanza kuwa hudumia kupata kibali na ardhi ya uwekezaji.

AIdha ameeleza kuwa, kituo hicho pia huwahudumia wajasiliamali wadogo kwa kuwajengea uwezo , kuwapatia mafunzo na kuwa unganisha na wewekezaji wakubwa .

Amesema Tanzania inazo fursa nyingi za uwekezaji na ili kujifunza zaidi wananchi wanashauriwa kutembelea banda la TIC , lililopo banda la Karume stand namba moja. 

No comments