Ads

UFUKWE WACHAFUKA , DC ILALA AONYA WANANCHI WAACHE KUTUPA TAKA MTONI




Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng'wilabuzu Ludigija  watatu mbele upande wa kushoto ,akishiriki zoezi la usafi maeneo ya ufuko wa Ocean road na Aga khan leo ,wakwaza mbele upande wa kushoto ni katibu tawala Wilaya ya Ilala Charangwa Makwiro (Picha na John Luhende )
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng'wilabuzu Ludigija  watatu mbele upande wa kushoto ,akishiriki zoezi la usafi maeneo ya ufuko wa Ocean road na Aga khan leo ,wakwaza mbele upande wa kushoto ni katibu tawala Wilaya ya Ilala Charangwa Makwiro na wakwanza upande wa kulia ni diwani wa kata ya Kivukoni Sharik Choughule

Baadhi ya watumishi wa Manispaa ya Ilala na Green west Pro  na boda boda  walijitokeza kushiriki zoezi la usafi wakiwa katika  picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija  

Baadhi ya watumishi wa Manispaa ya Ilala na Green west Pro  na boda boda  walijitokeza kushiriki zoezi la usafi wakiwa katika  picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija  


Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng'wilabuzu Ludigija  wa sita kutoka upande wa kushoto waliosimama na upande tatu upande huo ni katibu tawala Wilaya ya Ilala Charangwa Makwiro   ,akishiriki zoezi la usafi maeneo ya ufuko wa Ocean road na Aga khan leo ,aliye katikati mwa walio kaa ni Mkuu wa Idara ya Uhifadhi Mazingira na Udhibiti taka ngumu Manispaa ya Ilala Abdon Mapunda,  kutoka kwa DC  upande wa kushoto  ni diwani wa kata ya Kivukoni  Sharik Choughule,  wa kwanza  kushoto ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Green Waste Pro (LTD )Deusdedit Rutazaa wengine ni baadhi ya watumishi wa Manispaa ya Ilala na Green west Pro (Picha na John Luhende )

Mwamba wa Habari

Wananchi wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es salaam wametakiwa kuendelea kufanya usafi katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na kuepuka kutupa taka pembezoni mwa mto hususani msimbazi ili kutoviathiri viumbe vilivyo baharini.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es salaam na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng'wilabuzu Ludigija wakati akishiriki kwenye zoezi la usafi katika fukwe za bahari ya hindi katika maeneo ya Ocean Road pamoja na Agha Khan katika manispaa hiyo ikiwa ni kuunga mkono kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam aliyoitoa jumalilipita  ambapo alizitaka Manispaa zote za mkoa huo kufanya usafi. 

Ludigija amesema kutokana na zoezi la ufanyaji usafi kuonekana kuwa halikutiliwa mkazo hivyo ni vyema wananchi wakaendelea kufanya usafi wa kila Jumamosi ya Mwisho wa mwezi ili kujihadhari na magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na uchafu.

Amewakumbusha wananchi kuwa usafi ni wa kila mmoja hivyo wahakikishe kila mmoja kwa nafasi yake katika maeneo yanayomzunguka anafanya usafi na siyo kusubiri mpaka asukumwe na watu wa mazingira.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Uhifadhi Mazingira na Udhibiti taka ngumu Manispaa ya Ilala Abdon Mapunda,  amesema suala la usafi ni la kila mmoja hivyo amewasisitiza wananchi kuendelea kufanya usafi katika maeneo yao kwani itawasaidia kuweka mazingira yao katika hali ya usafi.

Mapunda amesema kurudishwa kwa zoezi hilo la ufanyaji wa usafi kwa kila jumamosi litasaidia kuleta hamasa kwa wananchi jambo litakalosaidia waepukane na magonjwa ya mlipuko ,homa ya matumbo ,kipindupindu na  kuhara.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Green Waste Pro (LTD )Deusdedit Rutazaa amewakumbusha wananchi kuwa taka sio suala la kampuni hiyo ya usafi pekee bali wahakikishe wanazihifadhi katika mifuko lakini pia walipe tozo za taka kwa wakati.

Hata hivyo Imeelezwa kuwa licha ya Manispaa ya Ilala kuzindua kampeni za ufanyaji wa usafi hii leo bado wananchi wataendelea kuhamasishwa kuzingatia ufanyaji wa usafi kwa kila Jumamosi ili kuifanya manispaa hiyo kuwa ya mfano wa kuigwa.

No comments