NLD WAKUTANA KUMJADILI MWENYEKITI ALIYEMPIGIA DEBE MAALIM SEIF ZANZIBAR.
Chama Cha
Upinzani nchini Tanzania National League for Democracy (NLD) kimepinga kauli ya
Makamo Mwenyekiti upande wa Zanzibar Bw. Hamadi Hemedi ambaye aliyedai kuwa
watamuunga mkono mgombea wa urais wa Chama cha ACT- Wazalendo Maalim Seif
Sharifu Hamadi.
Chama hicho kimeeleza
kuwa msimamo wao watampigia kura mgombea wao Mfalme Hamisi Hassan katika nafasi
ya urais Zanzbar katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 28 mwaka
huu.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Chama Cha NLD
Tanzania Bara Tozy Matwanga, amesema kuwa leo Oktoba 18 mwaka huu, kamati kuu watakaa kikao kwa ajili ya kumpa nafasi Bw.
Hemedi aweze kujieleza kwa sababu gani ametangaza kumuunga mkono maalim seif
bila kuwa na makubaliano na uongozi wa chama.
Bw. Matwanga
amesema kuwa chama cha NLD hawana mpango wa kushirikiana na vyama vyengine vya upinzani kama ilivyokuwa katika uchaguzi wa mwaka 2015
kwa sababu hawaoni faida zaidi ya kuwanufaisha baadhi ya vyama.
Katika hatua
nyengine amebainisha kwa sasa Mwenyekiti wa Chama cha NLD ni Taifa Bw. Mfalme
Hamisi Hassan na sio Bw. Oscar Makaidi kama ilivyokuwa inafahamika na watu
wengine.
Bw. Matwanga
amewataka watanzania kuwa na busara katika kuhakikisha uchaguzi mkuu unafanyika
kwa salama na amani, kwani kuna baadhi ya wagombea wamekuwa wakitoa lugha za
kuwachonganisha jambo ambalo sio rafiki.
“Tunawaomba watanzania
kujiepusha na wanasiasa wanaotumia lugha za uchochozi katika kipindi hiki cha
kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 28 mwaka huu ” amesema Bw.
Matwanga.
Bw. Matwanga
amempongeza Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli baada
kufuraishwa na utendaji kazi wake ikiwemo
ujenzi wa miundombinu ya barabara.
‘’Rais
amefanya mambo mengi mazuri katika kipindi
cha miaka mitano ya uongozi wake” amesema Bw. Matwanga.
Mwenyekiti
wa Idara ya vijana Taifa Chama cha NLD
Othiniel Mizizi, amesema kuwa wamejipanga kikamilifu kushiriki uchaguzi
mkuu pamoja na kuendelea kuomba kuwe na amani katika uchaguzi huo.
Post a Comment