Ads

KIGAMBONI YAPITISHA AZIMIO KUPONGEZA RAIS KWA MAPAMBANO DHIDI YA COVID 19

DC SARA MSAFIRI ASIMULIA MAZITO ALIYOYASHUHUDIA - YouTube

Mwamba wa habari

Baraza la Madiwani  Manispaa ya Kigamboni  kwa kauli moja  liemepitisha  azimio la Kumpongeza  Rais   Wa  Jamhuri Ya  Muungano  Wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Kwa Namna Alivyoliongoza Taifa  Katika Mapambano Dhidi Ya Janga la UgonjwaWa Corona (Covid-19)


"Katika  kukabiliana  na  ugonjwa   wa Corona  Rais alitumia mbinu na mikakati mbalimbali ikiwemo  kukataa    kuiga  mtindo na mbinu ya   kufunga mipaka  na  kuwafungia  wananchi  wake wasitoke nje tofauti na viongozi wa Mataifa mengine waliofunga  mipaka  ya nchi zao na  kuzuia watu wao kutokanje    (Lockdown) "Alisema DC Msafiri.

Aidha  alisema kwa  kuzingatia hali hiyo, Rais Magufuli  aliruhusu  shughuli za kiuchumi  na  baadhi  ya  shughuli za kijamii    ziendelee  kwa  tahadhari  na  kuwahimiza wananchi kuzingatia  maelekezo na miongozo  ya wataalam.

''Waheshimiwa Madiwani sipati picha ikiwa ingewekwa lockdown wananchi wetu hapa kigamboni ingekuwa maana shughuli zao zinategemea hadi wavuke upande wa pili wapate chakula  au pata picha Dar es salaam hatulimi magari yote kutoka mikoani yanayoleta chakula yangezuiwa tungekula nini hali ingekuwa mbaya sana"Alisema 

Wakitoa michango ya ya mawazo kuhusu mjadala wa  azimio hilo baadhi ya Madiwani  akiwemo  Diwani wa kata ya Tungi aliesema Rais Magufuli amesaidia kuwaondoa hofu  Watanzania Diwani wa kata ya Kigamboni Dotto Msawa , alitoa pongezi kwa kuruhusu ibaada huku Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kigamboni Maabadi Suleimani Hoja akisema Rais Magufuli amekuwa Mzalendo wa Kweli kwa Taifa.

No comments