Ads

SERIKALI YAKABIDHI HATI YA KIWANJA ALICHO AHIDI RAIS MAGUFULI KWA TAASISI YA AL-HIKIMA FOUNDATION.


 Image result for picha za alhikima

Na John Luhende 
Mwamba wa habari
Serikali imeitaka taasis ya Al-hikma Foundation  ,kulitumia kwa makusudi yaliyokusudiwa  eneo walilopewa na serikali  na kwamba Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  alitoa eneo hilo kwa immani ya kusaidia katika maendeleo kwa jamii.
Hayo yamesemwa na waziri wa  maliasili na utalii Mhe. Hamis Kigwangala   alipo mwakilisha Waziri mkuu Kasim Majaliwa ,katika   makabidhiano ya hati ya kiwanja  namba 118 Block  E Temeke ,  kilicho tolewa na Rais Magufuli kwa taasisihiyo ambapo walikiomba katika mashindo ya ya Afrika ya kusoma qurani yaliyofanika uwanja wa taifa mwezi mei 2019.
Alisema serikali  serikali ilirdhia kutoa endeo hilo ambalo lilikuwa mali ya umma ili taasisi hiyo ijenge Hospitali kama ilivyo omba hivyo alisema lisibadilishwe  matumizi.
‘’Mheshimiwa waziri mkuu amenituma nisema kwamba  Rais anamatarajio makubwa  na taasisi hii , mali hii anayowapa  mtaenda kuitendea haki katika eneo hili kwa uaminifu wa hali yajuu  tusimwangushe  kama mlivyo andaa mashindano  ya qurani kwa ustadi wa hali ya juu kadhalika hapa mfanye kitu kinacho endana na hadhi hiyo “Alisema 
Aidha  Kigwangala aliwataka wanafunzi wanao soma  katika shule za Alhikima   na shule za umma kusoma kwa bidii , na kuwataka wazazi kupeleka watoto wao katika shule hizo  kwani zina matokeo mazuri  napia aliwatawanafunzi  pamoja na kusoma masomo ya dini kuto acha kusoma elimu dunia kwani kila elimu inaumuhimu wake.
Aliwataka waislamu na  watanzania kumuungamkono   na kumuombea Rais Magufuli  kwani anania ya dhati kuiletea nchi maendeleo na wajitokeze kwa wingi katika uchaguzi wa Serikali za mitaa  unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu kuchagua viongozi waadilifu wenye mfano wa Magufuli.
Kwa upande wake Rais wa Taasisi hiyo  Shekh  Sharifu  Abdullkadri ,amemshukuru Rais Magufuli kwa kutoa kiwanja hicho na kusema kuwa kila ijumaa wataendelea kumuombea Rais Magufuli na kuiombea nchi kwa ujumla .
Naye Mkurugenzi wa Taasisi hiyo ambaye pia ni Mhadhiri wa kamataifa  Shekh Nourdin Kishik ,alisema tangu wamepewa eneo hilo na Rais  mwezi mei  na kwamba walichelewa kuifanya hafla hii kwa kuwa walikuwa na majukumu mengi baada ya Ramadhani na baadaye kwenda hija  ,na kusema kuwa Taasisi hiyo inabahati na Rais Magufuli  kwa kuwa alisha wahi kuwa saidi kipindi cha nyuma  walipo zungushwa kupata eneo hilo .
‘’Baada ya kuzungushwa sana eneo hili wakati akiwa waziri wa Ardh na maba na maendeleo ya makazi  alituuliza kote mlikopita hamja ombwa rushwa  na si tulimwambia hatukuombwa labda kama tulitengenezewa mazingira hayo lakini hatukuambiwa wazi, kwa sisi Al- hikima  ambao tuna mfahamu tangu 2007 ,baada ya siku mbili wakati huo akatusaidia tuka pata usajili wa shule zetu na sasa ametupatia kiwanja hiki  tuna shukurusana  hatuna cha kumlipa ila  tuemuombea dua kubwa  Mungu ampe wepesi katika mambo yake “Alisema 
Awali akitoa salamu za  malezi wa taasisi hiyo kwa niaba ya Rais mstaa Ali Hassan Mwinyi ,Dkt Hussein Al Hassan Mwinyi alimshukuru Rais  Magufuli kwa wema alioitendea taasisi hiyo na kupongeza taasisi hiyo kwa kuendelea kuyafanya kuwa makubwa mashindano  ya quran na kutiza agizo la Mtume Muhama la kumlipa mtu aliye watendea wema  kwa kumuombea dua.



No comments