Makonda awajia juu watendaji wakwamishaji miradi ya maedeleo ya kimkakati aunda kamati ya kuangalia mwenendo
![Image result for PICHA ZA MAKONDA](https://i2.wp.com/zanzibar24.co.tz/wp-content/uploads/makonda-1.jpg?fit=800%2C445)
Hussein
Ndubikile,
Mwambawahabari
Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewakemea na kuwaonya watendaji wote
wanaokwamisha Miradi ya Maendeleo ya Kimkakati kwa kusema
wataobainika watachukuliwa hatua za kinidhamu na kuwajibishwa.
Aidha, Mkuu
huyo amesema ataunda Kamati itayokuwa na jukumu la kuangalia mwenendo wa miradi
yote ya kimkakati kwa kupokea taarifa kila baada ya wiki mbili ndani ya mwezi
lengo likiwa kuwabaini wanaokwamisha wachukuliwe hatua.
Hatua hiyo
imekuja siku chache baada ya Rais John Magufuli kutembelea miradi hiyo ikiwemo
ya Machinjio ya Vingunguti na Coco Beach na kukuta ujenzi ukiwa hauendelea
licha ya Serikali kutoa fedha za ujenzi.
Hayo
ameyasema jana katika Kikao cha kupokea msaada wa kusomesha watoto wa kike 100
wa kidato cha tano waliochaguliwa mwaka huu wanaochukua masomo ya Sayansi
kutoka kwa Balozi wa Nchi za Falme za Kiarabu.
Alisema miradi
yote ya kimkakati iliyokwama ujenzi inakwamisha na watendaji licha ya Serikali
huku akibainisha alishakaa vikao na watendaji hao kujua mwelekeo wa miradi ila
cha kushangaza pasipo sababu za msingi imesimama ujenzi hauendelei.
“ Nafanya
vikao na watendaji wangu nawasisitiza waharakishe miradi ikamilike laikini
wanashindwa kutekeleza Rais Magufuli amepita kuona maendeleo Machinjio ya
Vingunguti amekuta hakuna kinachoendelea ni aibu,” alisema.
Makonda
alisema watendaji wa mkoa huo wamemvua nguo na kwamba angekuwa haofii njaa
angeshajiuzulu nafasi yake kwani haipendezi watu wazima kufanya kazi kwa kusukumwa.
Alibainisha
kuwa miradi yote iliyokwama fedha zake ilishatolewa muda mrefu ukiwemo wa
Machinjio ulipewa Sh billion 12.5 na Ufukwe wa Coco Sh bilioni 14 ila cha ajabu
miradi hiyo imekwama licha watendaji kupewa maelekezo awali.
Alisisitiza
kuwa wapo madiwani waliogombea nafasi kwa ajili ya kujinufaisha kama ilivyokuwa
kipindi cha nyuma na kwamba wanapoona mambo yao hayaendi wanakawamisha miradi.
Aliitaja
miradi mingine inayokwamishwa ni Mradi wa Ujenzi wa Soko la Kisutu, Stendi ya
Mabasi-Mbezi na wa Magomeni huku akiwasisitiza kuwapuuza wanasiasa wakwamishaji
maendeleo.
Alifafanua
kuwa kamati atakayounda itafuatilia miradi ya kimkakati mwenendo wake na kwamba
watakaokuwamo wataleta taarifa za miradi hiyo kwa muda uliowekwa.
Aliongeza
kuwa mradi wa Ufukwe wa Coco unavyozidi kuchelewa ndi mapato yanavyozidi
kupotea na kuwataka Wakuu wa wilaya kuwa wakali kwenye maeneo yao miradi ikamilike
kwa wakati.
Pia alisema
ana mpango wa kupeleka pendekezo la kukabidhiwa miradi yote ya kimkakati ili
kuachana na wanasiasa wanaokwamisha miradi hiyo lengo likiwa kuunga mkono
juhudi za Rais Magufuli za kuwaletea wananchi maendeleo.
Post a Comment