Wanafunzi zaidi ya 100 Shule za Msingi kuchuana Mashindano ya Tahajia
Hussein Ndubikile
Mwamba wa habari
Wanafunzi
kutoka Shule ya Zaidi 100 wa Mikoa ya Dar es Salaam, Lindi na kwa mara
ya kwanza Visiwa vya Zanzibar watachuana katika Mashindano ya kutamka
herufi za maneno ya Kiingereza (Tahajia) yanayotarajiwa kuhitimishwa
Novemba 10 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Hayo
yalibainishwa jana na Mkurugenzi wa Taasisi ya Coconut, Frank Mush
ambapo alisema mashindano yamefunguliwa rasmi mwezi Agosti na kilele
chake kitafikia Novemba mwaka huu huku akisisitiiza washindi kumi
watakaopatikana wanatarajiwa kuwa mabalozi wa elimu ya usomaji
wakitarajia pia kupata mialiko kuiwakilisha nchi kaitika ngazi za
kimataifa.
" Shindano hili
litashirikisha shule za Seriakli, binafsi na wadau wote wa elimu na umma
kwa ujumla wake kwa mwaka huu yataanzia ngazi ya shule ambapo washindi
10 hupatikana kufuzu kimkoa," alisema Mushi.
Alibainisha
kuwa kutokana nawingi wa shule , mkoa wa Dar es Salaam kupitia Manispaa
za awali za kiutawala yaani Temeke, Ilala na Kinondoni zitafanya
mashindano ya kimkoa hivyo kufanya mikoa 5 ukijumlisha Zanzibar na
Lindi.
Mushi alisema
washindi 20 kutoka kila mkoa watafuzu mashindano ya kitaifa ili kupata
washindi 10 bora kutoka makundi mawili kulingana na ngazi za madarasa.
Alisisitiza
kuwa mwaka huu Coconut Foundation imeungwa mkono na mdahamini Mkuu wa
mwaka ambayo ni kampuni ya kuchapisha vitabu vya elimu ya ngazi zote
ijulikanayo kama Oxford University Press Tanzania na kwamba Kituo cha
Runinga cha ITV kitarusha mashindano hayo mubashara ili kuweza kumfikia
kila mwananchi.
Alifafanua
kuwa lengo la mashindano hayo ni kuifika mikoa yote huku akisisitiza kwa
mwaka huu lugha ya Kiingereza itatumika peke yake.
Pia
alisema usajili wa ushiriki utakoma rasmi wiki ya pili ya mwezi
Septemba hivyo taasisi inaendelea shule kujisajili kufanikisha shindano
hilo.
Kwa upande wake,
Meneja wa kampuni ya uchapishaji vitabu na kamusi nchini, Fatma Shangazi
alisema wameamua kudhamini kutokana na umuhimu wake kwa watoto katika
kuboresha uwezo wao wa kutamka na kusoma na kwamba zawadi za vikombe
vitatolewa kwa washindi wa mwisho.
Naye
Meneja Masoko wa Kituo cha ITV na Radio One, Ernest Dile alisema
wataendelea kushirikiana na Coconut Foundation kufanikisha mashindano
hayo huku akiziomba taasisi zingine kujitokeza kudhamini.
Post a Comment