Tuzo 32 za Tanzania Elimu Awards kushindaniwa Agosti 31 Dar es Salaam
Hussein Ndubikile
Mwamba wa habari
Jumla
ya Washiriki 70 wakiwemo wanafunzi, walimu, shule, serikali, taasisi
pamoja na wadau pamja na wadau wa elimu watachuana kuwania tuzo 32 za
Tanzania Elimu Awards (TEA) zitakazotolewa na Kampuni ya Elimu Solutions
Agosti 31 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Hayo
yalibainishwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa kamupi hiyo
Neitahn Swed ambapo alisema wameamua kuanzisha tuzo hizo kwa mara ya
kwanza kwa kutambua na kutahamini mchango wa walimu na wanafunzi katika
kujenga taifa bora wakati likielekea kwenye uchumi wa viwanda.
"
Hafla ya kutoa tuzo hizi itafanyika tarehe 31 siku ya Jumamosi kuanzia
saa 9 mchana mpaka saa 2 usiku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mheshimiwa
Suleiman Jafo," alisema Swed.
Alibainisha
kuwa TEA itatoa tuzo 32 kutoka kwenye vipengele 11 na kwamba vigezo
vitakavyoangaliwa ni ufaulu wa mitihani ya kitaifa kuanzia ngazi ya
elimu ya msingi hadi Kidato cha sita huku akisisitiza shindano hilo
litakuwa endelevu.
Swed
alisema washindi wa tuzo hizo watapatikana kutokana na takwimu
zitakazopatikana kwa kushirikiana na wadau pamoja na Kamati
waliyoichagua.
Alifafanua
kuwa tuzo hizo zipo kwa ajili ya kuchangia utamaduni na kutunza na
kutambua mchango wa wasomi, wabunifu na wadau kwenye sekta ya elimu hasa
wakati nchi ikielekea uchumi wa kati kupitia uchumi wa viwanda.
Kwa
upande wake, Mratibu wa TEA, Peter Mboye alivitaja vipengele
vitakavyoshindaniwa vikiwemo vya wanafunzi bora wa kike na kiume ngazi
ya msingi hadi kidato cha tano, wanafunzi bora kwa ujumla, walimu bora
kwa msingi na sekondari, wanafunzi wenye mahitaji maalum, taasisi bora
pamoja na wilaya zilizofanya vizuri katika ufaulu.
Naye
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni hiyo, Catherine Ndosi aliwashukuru
wadau waliofanikisha tuzo hizo na kuziomba taasisi zingine kujitokeza
kusapoti shindano hilo.
Mwakilishi
kutoka Kampuni ya Asas, Abdul Ally alisema wameamua kudhamini tuzo kwa
kuwa wanatambua umuhimu wa elimu na kwamba mwaka jana walitoa lita
300,000 kwa ajili ya kuboresha afya za wanafunzi wa Nyanda za Juu
Kusini.
Post a Comment