Ads

SIMBA KUTUPA KARATA YA KWANZA KOMBE LA MAPINDUZI

SIMBA kesho itakuwa kwenye mchezo wao wa kwanza wa kombe la Mapinduzi dhidi ya Chipukizi ambao mchezo wao wa kwanza jana walipoteza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Mlandege.

Simba wameanza maandalizi ya kujiaanda kwa ajili ya mchezo huo mara baada ya kuwasili Zanzibar wakiwa na kikosi cha kwanza.

Mratibu wa Simba, Abbas Ally amesema wanajua ushindani ni mkubwa wamejipanga kuweza kupata matokeo.

"Tumekuja na kikosi kamili kwa ajili ya kuleta ushindani na tuna imani tutafanya vizuri, mashabiki watupe sapoti," alisema

No comments