Ads

MWENYEKITI UWT ILALA: UKIDONDOKA KIBIASHARA USIKATE TAAMAA ONAHAWA.



Na John Luhende  
Mwamba wa habari
Mwenyekiti wa umoja  wa wanawake  CCM  (UWT) Wilayani Ilala, Amina Dodi ,amewataka wanawake Wilayani Ilala  kutokata tamaa   katika ujasiliamali kutokana na changamoto wanazo pitia bali ziwaimarishe kwa kuwaongezea uzoefu nakufikiri  zaidi kuzikifursa za kiuchumi.

Dodi , ametoa usahauri huo katika semina ya Ujasiliamali ya kufunga mwaka 2018 na kuukaribisha mwakampya  2019 , ambapo  amesema  kuwa umoja huo  upo imara   na umeendelea kupata wanachama wapya kila siku kutokana na kazi nzuri zinazo fanywa na Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania  Dkt John Pombe Magufuli na kusema kuwa  wanawake wa Ilala wataendelea kumuunga mkono kwa kufanya kazi .

“Ninyi akina Mama mnafikilia kupatatu  ,(kuwini ) maisha nipamoja na kupata elimu, naomba niwatake tuwe watu wa  wasomaji wa habari mbalimbali ,hata Trump  wa Marekani ,alidondoka kibiashara akaja akainuka baadaye ,tuangalie Reginard Mengi alikuwa na Gazeti  Alasiri akadondoka lakini hakukata tama,na kwenye uujasiliamali hutakiwi kukata tama wala usije ukalalamika sana kwamba mimi mbona nafanya kazi nadondoka  uwe makini tu nabiasharayako ukidondoka utanyanukatu naomba  wamama niwatie nguvu mwaka huu 2019 utakuwa na mafanikio”Alisema.

Amesema ,mwaka uliopita ulikuwa na mafanikio mengi  kwa upande wa  (UWT ) Ilala  na kwamba wameweza kutimiza malengo yao mengi  ikiwemo kupata hati ya kiwanja chao ambacho  wanakitafutia wawekezaji ili kuongeza kipato cha umoja,na pia wameweza kuimarisha chama na umoja ,na wamepata semina zakutosha kuhusu ujasiliamali na sasa wanaweza kuendesha siasana uchumi.

“Uchumi na saiasa vinakwenda sawa wanawake hawa tumewajengea uwezo wa kujiimarisha kiuchumi na wanaweza kufanya siasa safi ,unaweza kuwa na siasa lakini uchumi ukilegalega huwezi kufanikiwa, kwahiyo kwaniaba ya wanawake (UWT ) Ilala tunamshukuru Rais kwa kujenga uchumi na tunamuombea Mungu ampe Afyanjema  iliaweze kutekeleza mambo mengine mwaka huu 2019.

Katika semina hiyo wanawake hao wamefundishwa  mambo mbalimbali ikiwemo elimu juu ya  Mikopo, namna ya kuandika katiba ya vikundi ,na namna ya kubuni na kuanzisha biashara,Asha Johari ni katibu UWT kata ya  Gerezani yeye ameishukuru UWT ,Manispaa ya Ilala na  serikali kwa kutoa mikopo isiyo na riba ambayo imekuwa ukombozi kwa akinamama ukilinganisha na miaka iliyopita ambapo wanawake waliteseka kwa kutozwa riba kubwa.

“Tulikuwa tunapata mikopo kutoka kwa mabenk ambayo ilikuwa nariba kubwa  ya asilimia  kumi hadi kumi natano ya mkopo sasa tunafaidika na huu usio na riba na tunajivuni serikalli hii inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi, imemwokoa mwanamke kwa kiasi kikubwa “Alisema

Moja ya mambo ambayo yamerudisha nyuma vikundi  vingi nikuwa na katiba zisizo faa ,ambapo katika semina hiyo yametolewa mafunzo ya kuandika katiba ,Ktiba ni muhimu sana na kilakikundi kinahitaji Katiba kutokana na kutokuwa na ujuzi huu wa kuandika katiba vikundi vingi vimekwama kupewa mikopo kutokana na kukopi Ktiba za vikundi vingine .

“Kwamafunzo haya  majukumu yetu sasa kama viongozi ni kwenda chini kwa  kuwafundisha wanawake na hata vijana ambao hawana mafunzo haya nao tuta wasaidia ii wapate katiba bora ‘’Alisema Aziat  Salim Juma Katibu UWT  kata ya Buyuni.

Pamoja na hayo katika semina hiyo wanawake wameweza kujifunza   ni uthubutu wa kuanzisha biashara , kujiamini na kuwa na mtazamo wa mbele zaidi kibiashara na wamemshukuru Mwenyekiti kwa kuwapatia mkufunzi kutoka Uingereza ambaye pia amewaahidi kuwa yatfutia masoko ya bidhaa zao .

“Ninachoweza kuwashauri wanawake wajasiliamali wenzangu ni  kuviweka vituvyetu katika hali ya usafi zaidi viewe vya kisasa vinavyoweza kuuzika hadi masoko ya nje  nami nitashuka huko chini  katika matawi kuwaelekeza  ili waweze kuzingatia haya “ Alisema  Magreth Cheka katibu UWT kata ya Kipawa.













No comments