Ads

MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI LEO .

  Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Tulia Ackson akiongoza kikao cha thelathini na moja cha mkutano wa kumi na moja cha Bunge hilo leo Jijini Dodoma.
 Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt Harrison Mwakyembe akizungumza na Mwanamitindo wa kimataifa Bi.Flaviana Matata  wakati  alipomtembelea leo Bungeni Jijini Dodoma.
  Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Dkt.Khamis Kigwangala na Mbunge wa Karagwe Mhe.Innocent Bashungwa wakiwa pamoja na Mwanamitindo wa Kimataifa Bi.Flaviana Matata katika viwanja vya Bunge leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe.Hamad Masauni akijibu maswali mbali mbali ya wabunge wakati wa kikao cha thelathini na moja cha mkutano wa kumi na moja cha Bunge hilo leo Jijini Dodoma 
Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akimskiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Sera,Bunge,Ajira,Vijana na wenye ulemavu Mhe.Jenista Mhagama wakati wa kikao cha thelathini na moja  cha mkutano wa kumi na moja cha Bunge hilo leo Jijini Dodoma.
Picha zote na Daudi Manongi-MAELEZO, DODOMA.

No comments