Ads

TUCTA KUSHIRIKI SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KIVINGINE


Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Rehema Ludaga akizungumza kuhusiana na Kongamano siku ya wanawake, jijini Dar es Salaam.

Mwamabawahabari
SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) imeandaa kongamano la siku ya wanawake litakalofanyika machi 7 jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake wa TUCTA, Rehema Ludaga amesema kongamano la  hilo ni kuelekea siku ya wanawake duniani ambayo inafanyika kila Machi 8.

Amesema kuwa katika kongamano hilo watajadili nafasi ya mwanamke katika mahala pa kazi kuona changamoto gani wanakutana wanawake wakiwa sehemu za kazi.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni Tathimini ya Unyanyasaji wa kijinsia mahala pakazi.

Katibu Mkuu waTUCTA, Dk.Yahya Msigwa amesema kila mwaka wanafanya kongamano ila kuweza kupata mawazo ya wanawake na kuweza kuboresha sehemu za kazi.

 Mgeni Rasmi wa Kongamano hilo anatarajiwa kuwa Mkuu wa Wilaya, Sophia Mjema.


No comments