Ads

ZIARA YA WAZIRI MKUU MAJALIWA WILAYANI SERENGETI.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na  Mbunge wa Serengeti, Cha Marwa katika mkutano wa hadhara alipuhutubia kwenye uwanja wa Mbuzi katika mji mdogo wa Mugumu wialyani Serengeti Januari 18, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wazee baada ya kuwakabidhi vitambulisho vya kuwawezesha kupatiwa matibabu bure hospitall yoyote wilayani Serengeti. Makabidhiano Hayo yalifanyika  kwenye viwanja vya hospitali ya wilaya Serengeti Januari 18, 2018
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wananchi wakati alipowasili kwenye uwanja wa Mbuzi katika mji mdogo wa Mugumu kuhutubia mkutano wa hadhara Januari 18, 2018.Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima.
Wananchi wa mji mdogo wa wilaya ya Serengeti wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Mbuzi katika mji mdogo wa Mugumu Januari 18, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikagua chumba cha upasuaji wakati alipotembelea hospitali ya wilaya ya Serengeti akiwa katika ziara ya mkoa wa Mara Januari 18, 2018
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi kadi ya matibabu ya bure kwa wazee, Johaness Chacha, moja wa wazee 280waliopatiwa vitambulishbo hivyo vitakavyowawezesha  kutibiwa  bure popote wilayani Serengeti katika makabidhiano yaliyofanyika kwenye viwanja vya hospitali ya wilaya ya Mugumu Januari 18, 2018. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimshukuru Mhandisi, Andrea Nyantori ambaye alichanga shilingi milioni 10  katika  harambee ya papo kwa papo ya kuchangia ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Serengeti katika mji mdogo wa Mugumu, Januari 18, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea mchango wa shilingi milioni 10 kutoka kwa Mhandisi Andrea Nyantori kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Serengeti Januari 18, 2018
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Askari Magereza wa gereza la Tabora Moja wilayani Serengeti wakati alipotembela gereza hilo kukagua mradi wa ufugaji ng’ombe wa nyama na maziwa Januari 18, 2018.

Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

No comments