MAKONDA AKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA CHINA NI MREJESHO WA ZIARA YAKE NCHINI CHINA ASEMA VIWANDA 200 VITAJENGWA DAR KIMOJA KIKUBWA KULIKO VYOTE AFRIKA
Na John Luhende
Mwambawahabari
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda leo amekutana na
ugeni wa wawekezaji kutoka China kujadilia na kuhusu mambo ya uwekezaji.
Akizungumza
katika mkutano huo Mhe. Makonda amesema kutokana na malengo yaliyo we kwa na
Wizara ya TAMISEMI maelekezo kutoka kwa Rais John Pombe Magufuli
kuwa kila mkoa uhakikishe unajenga viwanda 100.
Wawekezaji
hawa wanakwenda kuwekeza Tanga na kunduchi Dar es Salaam na Wana wekeza miradi
yenye thamani ya Dola bilioni 3dola.
Aidha
amewataka wanachi wa mkoa huo kuchangamkia fursa za uwekezaji.
"sisi kazi yetu kama serikali ni kuweka mazingira ya uwekezaji na hawandugu zetu wametoka jimbo la nilizungumza nao nilipotembelea huko kwao mwakajana"Amesema Makonda.
Pamoja
na hayo Makonda ameeleza kuwa Kuna clip ina zungunguka mtandaoni ikieleza kuwa
Ethiopia kuwa Wana kiwanda kikubwa zaidi kuliko nchi zote barani Afrika na
kusema kuwa wananchi wasihofu kwani Dar es Salaam itajenga kiwanda kikubwa
zaidi ya mara tatu ya hicho chenye Siguare mita Milion Tano na uwekezaji huu
utafanyika wilayani Kigamboni.
"Kuna
mwekezaji mwingine ameonyesha nia ya kuwekeza kiwanda cha sukari Nawaomba
wafanyabiashara wetu mchangamkie fursa hizo za kibiashara na vijana
pia mchangamkie fursa za ajira" Amesema Makonda.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa jimbo la Gwangzou , Xie zhenghy kutoka China amesema
wao wako tayari kwa uwekezaji na katika nchi ambazo zitaendana kiutamaduni kama
ilivyo kwa Tanzania.
Hata
hivyo amesema kuwa China imekuwa na nafasi kubwa ya kuwekeza barani Afrika
ambapo imekuwa na uwekezaji mkubwa nchini Misri.
Akizungumzia
uwekezaji hapanchini amesema kuwa uwekezaji watakaofanya ni ule unaendana na
kaulimbiu ya Rais John Pombe Magufuli.
Post a Comment