YANGA YAWASILI NA BOTI DAR KIMYA ! KIMYA, MASHABIKI WAMTUPIA LAWAMA CHIRWA.
MWAMBA WA HABARI
NA NOEL RUKANUGA, DAR ES SALAAM.
Baada ya kupoteza mchezo wa nusu fainali kombe la Mapinduzi dhidi
ya URA ya Uganda kwa michwaju ya penati, klabu ya Yanga imewasili jijini Dar es
Salaam wakitokea viziwani Zanzibar huku mashabiki wa soka wakipeleka lawama zao
kwa mshambuliaji wa Kimataifa Mzambia, Obrey Chirwa.
Sauti za mashabiki wa soka walisikika wakisema ahsante Chirwa, huku
wengine wakibeba mabango yenye ujumbe wa ‘AHSANTE CHIRWA) jambo ambalo
lilipelekea mchezaji huyo wa kimataifa raia zambia kupewa ulinzi wa kutosha.
Hali
inakuja baada ya Chirwa kukosa penalti ya mwisho ya Yanga baada ya wenzake wote
wanne kupata ambao ni Mkongo Papy Kabamba Tshishimbi, na wazalendo Hassan
Ramadhani Kessy, Raphael Daudi Lothi pamoja na Gardiel Michael Mbaga katika
mchezo wa nusu fainali uliopigwa jana.
Mshambuliaji wa Kimataifa wa Yanga Mzambia, Obrey Chirwa akiwa amezungukwa na mashabiki wa soka jijini Dar es Salaam.
Katika mchezo huo Chirwa aliingia
kipindi cha pili kwenda kuchukua nafasi ya Pius Buswita ili kuongeza nguvu safu
ya ushambuliaji ya Yanga, lakini Mzambia huyo alishindwa kucheza vizuri
kutokana na kile kilichoonekana wazi hakuwa fiti.
Chirwa alikuwa kwao Zambia
kufuatia mgomo wake wa kushinikiza alipwe fedha za usajili na amerejea juzi Dar
es Salaam na moja kwa moja kusafirishwa kuletwa Zanzibar kabla ya kuingizwa
uwanjani kipindi cha pili.
Hata hivyo penalti aliyokwenda
kupiga ilikuwa ya ovyo kabisa na kipa wa URA hakuhitaji kujisumbua kuiokoa,
kwani mpira ulimkuta mikononi tena pale pale aliposimama.
Kocha Msaidizi wa Yanga Shadrack Nsajigwa akizungumza na waandishi wa habari.
Baadhi ya Mashabiki wa soka.
Akizungumza na
waandishi wa habari baada kuwasili jijini Dar es Salaam, Kocha msaidizi wa Yanga
Shadrack Nsajigwa amesema kuwa
kikosi chake kimepambana na kuweza kuishia katika hatua ya nusu fainali.
Amesema kuwa
lengo lao lilikuwa ni kuchukua kombe lakini katika mpira lolote linaweza
kutokea.
Akizungmuzia
mcheza wao wa kimataifa Mzambia Chiwra ambaye alikosa penati ya mwisho na
kusababisha kutolewa nje katika mashindano hayo na URA ya Uganda, amesema hakuwa
fiti katika mchezo huo.
Amesema kuwa
kuna uwezekano siku hiyo hakuwa vizuri kwani katika mchezo lolote linaweza
kutokea.
Yanga SC
imepanda boti na kurejea mjini Dar es Salaam baada ya kutolewa kwenye michuano
ya Kombe la Mapunduzi kwa penalti 5-4 na URA ya Uganda kufuatia sare ya 0-0 ndani
ya dakika 90 katika Uwanja wa Amaan, Zanzibar hapa januari 10 mwaka huu.
Hatua hiyo imebainisha kuwa Yanga SC imeendeleza utamaduni wake wa kufanya
vibaya kwenye hatua ya matuta baada ya mshambuliaji wake Mzambia, Obrey Chirwa
kumdakisha mpira kipa wa URA, Alionzi Nafian.
Chirwa alikosa penalti ya mwisho ya Yanga baada ya wenzake wote wanne, Mkongo
Papy Kabamba Tshishimbi na wazalendo Hassan Ramadhani Kessy, Raphael Daudi
Lothi na Gardiel Michael Mbaga kufunga.
Katika mchezo huo uliochezeshwa
na refa Issa Hajji, aliyesaidiwa na Shehe Suleiman na Mwanahija Makame, penalti
za URA zilifungwa na Patrick Mbowa, Enock Kigumba, Shafiq Kagimu, Jimmy Kulaba
na Brian Majwega.
Katika dakika 90 za mchezo timu
zote zilishambuliana kwa zamu, ingawa URA ndiyo walioonekana kulitia misukosuko
zaidi lango la Yanga.
Kufatia matokea Matajili Azam Fc
wataminjana na URA katika mchezo wa
fainali utakaopigwa huku visiwani Zanzibar.
Post a Comment