Ads

WAZAZI MBURAHATI SACCOS YAZINDULIWA RASMI , MWENYEKITI JUMUIYA YA WAZAZI MKOA WA DSM AITAKA NMB KUPUNGUZA RIBA.





Mwambawahabari 
Na. john Luhende
Wanachama  wa Chama cha Mapinduzi CCM  na wananchi  wa mkoa wa Dar es salaam wametakiwa kujiunga katika vyama vya kuweka na kukopa SACCOS ilikujikwamua kiuchumi   na kuondokana na hali ya utegemezi .
Hayo yamesema  na mwenyekiti wa jumuiya ya Wazazi mkoa wa Dar es salaam  Frank  Kalokola Kamugisha  wakati wa  uzinduzi wa chama cha kuweka na kukopa  ,  (Wazazi Mburahati SACCOS) uliofanyika katika  ukumbi wa  Simba Oil Mburahati   jijini Dar es salaam, na akawataka wanachama  wengine wa chama hicho  katika maeneo mbalimbali  kuiga mfano wa Mburahati.

‘’Mstarajie kuwa ukiweka pesa leo na kuitoa kesho  kwa mbautapata kitu ,wekezeni kwa wingi ili muweze kukopa fedha  za kufanya maendeleo katika biashara  zitakazo wainua kiuchumi na siyo  kuzitumia kwa starehe au mambo yasiyo ya maendeleo” alisema Kamugisha .

Aidha  amewashukuru wadhamini wa Mkutano huo  Benk ya NMB kwa  kupunguza masharti ya kufungua akauti na kupunguza riba kutoka 3% hadi 2.5%  ili wanachama wa SACCOS hiyo waweze kufaidika  na Ushirika huo.
Amesema  katika kutekeleza  Ilani ya Chama kuwa kila kata  kuwa na SACCOS  yake  itakayo  wawezesha wanachama na wananchi  wasiona mitaji kuweza kuweka na kukopa  fedha zitakazowasaida  katika biashara kwa maendeleo binafsi na taifa kwa ujumla.
Wazazi Mburahati  SACCOS , ilianzishwa mwaka  20/Juni 2017 na kupata usaji wake  Novemba 2017 kwa  usajili namaba DSR 1647, ikiwa na nawanachama 90 na sasa inawanachama300 , akisoma Risala kwa mgeni Rasmi katibu wa Wazazi Mburahati  Engilibert  Nyang’ali  amesema,  ushirika huo umelenga kutoa mafunzo kwaviongozi na wanachama  juu ya namna bora ya  kusimamia uendeshaji kwa kupitia semina  ili kuweza kujua  haki na wajibu wao na kutoa mafunzo ya  ujasilia mali kwa wanachama wote.
Kwa upande wake afisa ushirika wa Manispaa ya Ubungo  Philipo Emmanuel, amewataka viongozi wa Ushirika huo kuwa waadilifu kwa fedha za wanachama na kueleza moja ya changamoto katika jamii nielimu kuhushu vyama vya kuweka na kukopa kwa kuwa wananchi  wengi hawana elimu ya kutosha .

“Nimekuwa najiuliza kwanini wazungu wanaungana  na kuwa na umoja ? nikagundua kwa  wanaamini nkatika umoja kuwa ni nguvu na mabo yakifanyika kwa umoja yanafanikiwa  nashukuru Wazazi  Mburati kwa  kuzuanzisha Ushirika huu”Alismema  Philipo.

No comments