MOHAMED SALAH MCHEZAJI BORA AFRIKA.
MWAMBA WA HABARI.
Nyota wa timu ya
Liverpool raia wa Misri, Mohamed Salah aliyekuwa akichuama na Pierre-Emerick
Aubameyang, na Sadio Mane katika kinyang'anyiro cha kuwania tuzo ya mchezaji
bora kwa mwaka 2017, usiku wa kumkia leo ametangazwa kuwa mchezaji bora wa mwaka
2017 wa Shirikisho la soka barani Afrika.
Salah
alionekana kuitetea vyema timu yale ya Liverpool mnamo mwaka jana 2017
baada ya kujipatia goli 23 katika mechi 29 baada ya kujiunga katika ligi kuu ya
Uingereza akitokea timu ya AS Roma.
Wapinzani
wake nao si haba kwani Pierre-Emerick Aubameyang, wakati huo huo, alifunga
mabao 31 ya kipekee kati ya michezo 32 katika mashindano yote ya mwisho.
Tuzo hiyo ya shirikisho la soka barani
Afrika ilikuwa na orodha ya wachezaji wapatao 24, miongoni mwa hao watatu mwezi
Desemba Salah, Aubameyang na Mane walitangazwa kuingia katika hatua ya mwisho
ya tatu bora .
Mshindi wa tuzo hiyo kwa mwaka uliopita
alichaguliwa na makocha kwa kushirikiana na manahodha wa timu katika kila timu
ya wanaume barani Afrika.
Sadio Mane kutoka katika timu ya
Liverpool amekuwa mshindi wa pili kwa wingi wa kura, pamoja na nyota mchezaji
wa timu ya Dortmund ,aubameyang kushika nafasi ya tatu kwa wingi wa kura.
Post a Comment