Ads

MANISPAA YA KINONDONI KUJENGA KIWANDA CHA KISASA CHA KUCHAKATA TAKA ,WACHINA WAPEWA TENDA.

Mwambawahabari
 Meya wa Manispaaya Kinondoni Benjamini Sitta kulia akishuhudia Meneja wa kampuni ya CRJE  Bwana Haochen akisaini mkataba tayar kwa kuanza ujenzi wa kiwana cha kuchata taka(picha  zote na John Luhende, wa mwambawahabari)

Halmashauri ya  Manispaa ya Kinondoni  leo  imesaini mkataba wa ujenzi wa kiwanda cha kuchakata   taka  kuzibadilisha kuwa mbolea    kitakachojengwa na kampuni ya CRJE ya nchini China  ambapo ujenzi huo unatarajia kuanza kesho.


Akizungumza na waandishi wa habari  katika tukio la  kusaini mkatabahuo, Meya  wa Manispaa hiyo ,Benjamini Sita amewaeleza  kuwa kusainiwa kwa mkataba huo itasaidia kuweka maeneo ya manispaa hiyo kuwa safi ,na mbolea aina ya mboji itakayozalishwa na kampuni hiyo itakuwa rafiki kwa udongo na mazingira kwani haina kemikali .

Aidha ,  amesema kuwa  kujengwa kwa kiwanda hicho kitaongeza ajira kwa wananchi pia kitawasaidia wakulima kutumia mbolea ambayo ni bora na ya kisasa huku ikiwa haina athari kwa udongo na hata mazao.
Pamoja na hayo sitta amaesema kuwa , kupitia mkataba huo manispaa ya Kinondoni itakuwa imeunga mkono kiasi kikubwa jitihada za Rais Magufuli katika kuelekea Tanzania ya viwanda, hivyo wananchi watapata ajira itakayo wasaidia kujikimu kimaisha .

No comments