ADHABU YA KIFO YAPINGWA MAHAKAMANI ,LHRC YASEMA INAKIUKA HAKI ZA BINADAMU
Na John Luhende
Mwambawahabari
Kituo cha sheria na ham za binadamu LHR ,kimetoa tamko kulaani na kuomba adhabu ya kifo ifutwe kwa kuwa imekua ikiathiri kwa kiwango kikubwa haki ya msingi ya kuishi kwa kuwa ni adhabu inayo inayo dhalilisha utu wa binadamu.
Kituo cha sheria na ham za binadamu LHR ,kimetoa tamko kulaani na kuomba adhabu ya kifo ifutwe kwa kuwa imekua ikiathiri kwa kiwango kikubwa haki ya msingi ya kuishi kwa kuwa ni adhabu inayo inayo dhalilisha utu wa binadamu.
Akisoma tamko hilo Leo katika kuadhimisha siku ya kupinga adhabu ya kifo duniani mbele ya waandishi wa habari mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho Bi Hellen Kijo Bisimba , amesema ,wakati umefika Sasa kwa Tanzania kuachana na adhabu hiyo kwa kuwa hata waingereza walio ianzisha tayari wamesha achana nayo, serikali itekeleze pendekezo la tathimini ya haki za binadamu ya umoja wa mataifa kwa kuridhia mkataba wanyongeza wa haki za kiraia na kisiasa na kutangaza rasmi Sasa kuwa adhabu hiyo haitekelezeki.
Aidha ameitaka serikali kurekebisha sheria ya kanuni na adhabu na sheria ya ugaidi yenye kutoa adhabu ya kifo kwa makosa ya mauaji ,uhaini na ugaidi.
Vilevile amesema serikali ibadilishe sheria na kuondoa adhabu ya kifo na kuweka adhabu mbadala kwenye akosa ya jinai na kwa wafungwa waliopo ,mfano vifungo vya muda mrefu gerezani .
Pamoja na hayo adhabu hiyo hapa nchi haija tekelezwa kwa muda mrefu ambapo hadi mwaka 2016 kulikuwa na watu 472 walio kuwa wamehukumiwa kunyongwa ambao kati yao 452 ni wanaume na wanawake 20 kati yahao wanao subiri kunyongwa ni 228 na wengine 244 bwana subiri maamuzi ya rufani zao , na sheria hiyo haija tekelezwa kwa muda wa miaaka 24 ya kwanza Uhuru buku watu 72 pekee wameshawahi kunyongwa yangu sheria hiyokanzishwa.
Pamoja na hayo kituo hicho kimefungua kesi mahakama Mkuu dhidi ya mwanasheria Mkuu wa Serikali kupiga adhabu hiyo na kuwataka wapigania haki kote nchini kuunga mkono juhudi hizo ili haki iweze kutendeka na kukomesha udhalilishaji huo wa haki ya msingi ya kila binadamu.
Post a Comment