Ads


Na John Luhende
mwambawahabariblog
Waandishi wa habari nchini  wametakiwa kuandika habari za kuelimisha jamii kuhusu masualambalimbali ya kuelimisha jamii  ikiwemo sector ya mafuta na gas badala ya kuandika habari za uchochezi wa migogoro katika jamii

Hayo yalisemwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  mh sadiq meck sadiq  alipo kuwa mgeni rasmi katika  ufunguzi wa semina semina  iliyo andaliwa na shirika la petrol Tanzania TPDC  kwaajli ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari  kuandika za ukweli kuhusu  sector ya mafuta na gas nchini .


 Naye mkurugenzi mkuu wa shirika hilo bw James Mataragio  amesema nijukumu la waandishi wa habari na wataalamu kuwaelimisha wananchi  kuhusu habari za maendeleo ya mafuta nagas nchini  , na ameongeza kuwa  watanzania wanatakiwa kuelewa kuwa  miradi ya mafuta na gas ni miradi mikubwa  na mtokeo yake yana onekana kwa muda murefu   na wawe wavumilivu .

Pamoja na hayo  alisema kuwa kwasasa ni takribani  viwanda 37 nchini  vinatumia nishati ya gas asilia  na taasisi mbalimbali  na hivi karibuni  mradi wa usambazaji wa  gas ya majumbani  kwa kutumia mabomba  utaanza na  nyumba 36000 zita patiwa huduma hiyo  kwa awamu ya kwanza



No comments