Ads

WANANCHI WAENDELEA KUNUFAIKA NA OFA ZA TTCL SABASABA 2026


Habari Picha 12830

Na Mwandishi Wetu
Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa Banda Janeth Maeda amesema ushiriki wa Shirika katika Sabasaba 2026 unalenga kuwasogezea wananchi huduma, kuongeza uelewa kuhusu bidhaa na huduma zinazotolewa na TTCL, pamoja na kujenga mahusiano imara na wateja na wadau mbalimbali.
Aidha, amebainisha kuwa maonesho hayo yanatoa fursa kwa Shirika kupokea mrejesho wa wateja ili kuendelea kuboresha huduma na kuendana na mahitaji ya soko la mawasiliano linalobadilika kwa kasi.
Habari Picha 12831
Aidha,wananchi na wadau wanaotembelea banda hilo wanapata fursa ya kutumia buree public Wi-Fi inayopatikana katika viwanja hivyo ili kufahamu speed ya intanet ya TTCL.
TTCL inaendelea kuwakaribisha wananchi wote kutembelea Banda la Shirika hilo katika Viwanja vya Mwalimu Julius  Nyerere ili kujionea teknolojia bunifu, kupata elimu kuhusu huduma za mawasiliano na kunufaika na ofa maalum zinazopatikana katika kipindi chote cha maonesho.
Habari Picha 12832

Pamoja na hilo, TTCL inaendelea kuwapatia wateja ofa maalum za Sabasaba, zikiwemo vifaa vya mawasiliano vinavyopatikana kwa bei zenye punguzo kubwa, pamoja na huduma mbalimbali zinazolenga kurahisisha maisha na shughuli za kila siku katika mazingira ya kidijitali.

No comments