Ads

Shirika la kupambana na unyanyasaji Kijinsia ''Mulika Community '' lazinduliwa







Na Heri Shaaban (CHANIKA)


SHIRIKA lisilo la kiserikali la kusaidia jamii na waathirika wa  unyanyaaaji kijinsia limezinduliwa rasmi na Mbunge wa Jimbo la Ukonga Jery Silaa. 


Akisoma taarifa ya shirika la Mulika Community Mwenyekiti wa shirika hilo Saida Mavumbi Ally alisema malengo ya shirika hilo kuwaunganisha waanga wa kijinsia zote na kuwapa mafunzo ya afya ya akili ,ikiwemo kutoa misaada  wa kisheria kwa ajili ya kulinda haki na utu wa Jamii husika .


"  Leo ni siku ya uzinduzi wa shirika letu la mulika linaloshughulikia maswala ya kikatili kijinsia  ambalo  litakuwa linaisaidia Serikali kukomesha vitendo vya kijinsia na ukatili kwa jamii pamoja na kuhamasisha na kutoa  tahadhari juu ya mabadiliko ya hali ya hewa pamoja na kuweka sawa mazingira ikiwemo kupanda miti katika taasisi za Serikali na shuleni "alisema  Saida 


Mwenyekiti Saida alisema pia majukumu yao mengine shirika hilo kutoa elimu mtambuka yenye kuleta tija  katika jamii iliyoathirika ili kutambua haki zao hususani haki za watoto wadogo ,haki za wafanyakazi majumbani ,ikiwemo kupata elimu na haki ya kupewa uhuru wa kwenda kuchagua viongozi. 


Pia alisema shirika la Mulika  dhumuni lao lingine kwa kusaidia jamii kuwajengea uwezo imara makundi ambayo yamepitia changamoto ya kutengwa na jamii na kuteswa vibaya ikiwemo vipigo na kunyimwa haki za msingi.


Akizungumzia mikakati ya shirika hilo katika kusaidia jamii ikiwemo kutoa mafunzo ya ukatili wa kijinsia na kutunza mazingira, pamoja na kutoa mafunzo ya ujuzi  wa ushonaji nguo utengezaji wa batiki ,ususi na urembo.


"Shirika letu pia linahamasisha matumizi ya Nishati safi ya kupikia kwa jamii na kutoa mafunzo ya cherahani kwa wasichana na watu wenye ulemavu wa ngozi ,wajane kwa muda wa miezi mitatu kwa wanufaika 600"alisema 


Mbunge wa Jimbo la Ukonga Jery Silaa,alipongeza Shirika hilo ambalo lipo jimbo la Ukonga litasaidiana na Serikali katika kukomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa jamii ambapo alisema atawasaidia kutafuta wadau shirika liweze kufikia malengo yake.


Mbunge Jery Silaa alikabidhi kompyuta kwa ajili ya shughuli za taasisi hiyo na kuwataka wachape  kazi   katika kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa watoto na jamii kwa ujumla


No comments